Skip to main content

Msome hapa Chini Ramsey anavyofunguka!!



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Ramsey Nouah amesema, amepitia vipindi mbalimbali vigumu katika maisha yake kabla ya kuibuka kuwa mcheza filamu mahiri nchini humo.
Ramsey, mmoja wa wacheza filamu wanaolipwa pesa nyingi nchini Nigeria, alisema hayo hivi karibuni alipohojiwa na gazeti la The Sun News la nchi hiyo.
Mcheza filamu huyo mwenye mvuto na ambaye ni mahiri kwa kucheza filamu za mapenzi, amesema kuna wakati alikaa bila kula kwa siku tatu hadi nne ikiwa ni pamoja na kuishi mitaani.
"Kuna wakati, wakati ule wa matatizo, hatukuwa na kitu, tuliishi kwa matatizo. Tulikuwa tukisaidiwa na watu. Kuna wakati tulishinda njaa kwa siku tatu hadi nne,"amesema mcheza filamu huyo mwenye mke na watoto wawili.
"Unashinda na njaa, tumbo lako halina kitu, lakini huna pa kwenda. Kuna wakati niliishi mitaani na kwenye maduka. Kuna wakati nilikuwa nalala chini ya daraja," aliongeza mcheza filamu huyo.
Ramsey amesema bahati nzuri ni kwamba hakuna kumbukumbu za maisha hayo ya dhiki aliyopitia, lakini huwa anayakumbuka vyema kila anapokumbuka alikotoka.
Mcheza filamu huyo mwenye mvuto amesema anashukuru kwa kupitia maisha hayo, ambayo kuna wakati yalimfanya amchukie kila mtu aliyekuwa karibu naye.
"Kiukweli, nilizoea kujiuliza kwa nini Mungu ananifanyia hivi? Lakini nafikiri Mungu alielewa kwamba, nilihitajika kuishi hivyo kwa ajili ya maisha yangu ya baadaye,"amesema Ramsey.
Mcheza filamu huyo amesema, watu wamekuwa wakiyatafsiri vibaya maisha yake kwa kumuona anaringa, lakini ukweli ni kwamba ni mtu wa kawaida na asiyependa kujikweza.
"Mara nyingi watu wengi wamekuwa wakinishutumu, lakini nikiwa mwigizaji, napaswa kukabiliana na mambo haya. Na ni rahisi kwa watu kunisema kwa sababu hakuna aliyevaa viatu vyangu.
"Wanigeria ni wepesi wa kuhukumu kwa sababu ni wazuri katika kusema maneno kabla ya kufikiri. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba sisi ni binadamu wa kawaida kama walivyo wengine. Mimi si Yesu na sipo hapa kuiokoa dunia,"amesema Ramsey.
  Amesema kuwa kwake muigizaji hakuna maana kwamba, amekuwa akipata kila anachokihitaji ama kuwa na maisha mazuri. Amesema watoto wake wamekuwa wakiugua na kupelekwa hospitali kama watoto wengine.
Licha ya ukimya wa muda mrefu, Ramsey amesema bado anaendelea kucheza filamu na anamuomba Mungu fani hiyo ipige hatua kubwa kimaendeleo nchini Nigeria kuliko ilivyo hivi sasa.
Ramsey amesema licha ya mafanikio waliyofikia, wacheza filamu wa Nigeria hawana mafanikio makubwa na hilo limekuwa likiwaathiri na kuwafanya wasiwe na uhakika wa maisha yao ya baadaye.
"Kwa mfano, baadhi ya wacheza filamu wakongwe wamekufa wakiwa masikini na mazishi yao yalifanyika kwa kuchangiwa na watu kwa lengo la kuwapa heshima,"amesema Ramsey.
Ili kuifanya fani hiyo ipige hatua kubwa zaidi kimaendeleo nchini Nigeria, Ramsey amesema wanapaswa kutengeneza filamu za kiwango cha juu,ambazo zitadumu na kuwa na mvuto kwa miaka mingi.
"Lazima kuwepo na mabadiliko. Bila fani yetu kukua, hatuwezi kuwa na maisha mazuri.  Mashabiki wamechoka kuona kitu kilekile. Hii ndiyo sababu iliyonifanya niwe kimya kwa muda.
"Naipenda kazi ya uigizaji. Napenda kufanyakazi, ambayo italeta mafanikio katika fani. Napenda kucheza filamu, ambayo unaweza kuitazama kwa miaka mitano au 20 na kuifurahia. Nataka kuacha alama na kumbukumbu si kuuza sura,"amesema.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.