Skip to main content

MWAKA 2014 ULIANZA HIVI: MUME WA THEA AFUMANIWA LIVE NA MKE WA MTU ANGALIA HAPA KICHAPO KILIVYOTEMBEA...!



MWAKA ulianza vibaya kwa mke wa mtu ambaye jina lake halikupatikana mara moja kumkimbia mumewe na kumfuata mume wa msanii wa filamu, Ndumbangwe Misayo ‘Thea’ aitwaye Michael Sangu ‘Mike’ jambo lililosababisha ale kichapo cha nguvu na kuuanza mwaka mpya vibaya.


Tukio hilo lililovuta hisia za wengi, lilitokea siku ya mkesha wa mwaka mpya, usiku wa kuamkia Jumatano, katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni, Dar ambapo Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’ ilikuwa ikikonga nyoyo za mashabiki wake.
KAMERA ZA IJUMAA
Paparazi wetu aliyekuwa ukumbini humo alimuona Mike akiwa upande mwingine na washikaji zake huku wakiendelea kula raha wakati wa shangwe za mwaka mpya wakati mdada huyo ‘kibonge’ akiwa na mumewe na watu wengine wakifanya yao.
Ijumaa lilipata shaka kidogo, baada ya kumuona dada huyo akimwacha mumewe kila wimbo unapokolea na kwenda alipokuwa Mike kisha kucheza naye.

Harufu ya ugomvi ilianza kunukia mapema, baada ya paparazi wetu kumshuhudia mume wa dada huyo akionekana kumkaripia japo kwa sauti ndogo mkewe kila aporudi akitokea kucheza na Mike.
ONYO HALIKUZAA MATUNDA
Pamoja na onyo alilokuwa akitoa mume huyo kwa mkewe mara kwa mara, bado dada huyo alionekana kumfuata Mike na kucheza naye tena kwa ukaribu kama vile wanajuana.
Baadaye jamaa huyo aliamua kuwashirikisha marafiki aliokuwa amekaa nao meza moja kuhusu tabia ya mkewe, wakamsihi asiende tena kucheza lakini bado hakusikia.
“Sisi tulimwambia, mwenzako hataki uende kucheza na yule msanii, anahisi labda kuna kitu kinaendelea lakini hakusikia, sijui ni pombe zilimzidi au vipi,” alisema mmoja wa watu waliokuwa wameketi meza moja na wanandoa hao muda mfupi baada ya tukio la kichapo kutokea.


Akaongeza: “Kuna wakati alikuwa akijifanya ameelewa, lakini sasa alikuwa akiaga na kujifanya anakwenda msalani halafu mumewe akifuatilia anagundua kumbe amemfuata Mike ili wacheze, jamaa akachukia sana.”
KICHAPO
Baada ya mume kuona dharau za waziwazi zikifanywa na mkewe mbele ya watu aliokuwa amekaa nao, aliamua kusimama na kumfuata alipokuwa akicheza na Mike.
Hakuwa na haja ya kuuliza chochote, alimkamata mkewe na kuanza kumshushia kichapo cha nguvu huku wengi wakiendelea kuponda raha kama vile hakuna kilichotokea.

“Ni mke wake? Hizo ni dharau, acha apigwe. Hawa wanawake wa Dar ni wajinga sana. Utamwachaje mumeo uende kushobokea wasanii? Huu ni upuuzi. Ni haki ale kichapo,” alisikika akisema jamaa mmoja aliyekuwa jirani na paparazi wetu.
DAMU CHAPACHAPA
Hasira zilipompanda yule jamaa, hakuchagua mahali pa kupiga, alimvuta nywele na kumpiga makonde kila sehemu ya mwili wake hali iliyosababisha damu imwagike chapachapa (angalia picha ukurasa wa mbele).
Mashuhuda walipoona damu imemwagika ndipo wakaingiwa na huruma na kuamulia ugomvi huo.
UTETEZI WA MKE
Katika kujitetea, mwanamke yule alimlaumu mumewe kwa kumpiga hadi kufikia kutoa damu kwa kosa la kucheza na Mike akisema kwamba, haoni kosa lake.
“Mume wangu unanionea tu bure, huyu sina uhusiano naye wowote ule... nacheza naye tu kama marafiki. Simfahamu na wala sijawahi kumuona zaidi ya kwenye filamu,” alisema mwanamke huyo.
MIKE HUYU HAPA
Kwa upande wa Mike, alipoulizwa na mwandishi wetu kuhusu kisanga hicho alisema, anamshangaa jamaa mwenye mke kwa sababu amemuonea mkewe bila sababu ya msingi.


“Kuna kosa gani watu kucheza muziki? Hapa ni ukumbi wa muziki, tena usiku. Hakuna mipaka, yeyote anaweza kucheza na yeyote. Ule mimi naweza kusema ni ulimbukeni wa kutojua mambo.
“Amemuonea... yule dada alikuwa anafurahi tu sherehe za mwaka mpya ambapo staili yake ya kucheza labda imemkera mumewe lakini kama alikuwa hataki mkewe acheze na mtu mwingine, si wangekaa tu chumbani kwao wawashe redio wacheze wawili tu kuliko kuja kuleta kero kwenye kumbi za burudani?” alisema Mike.
Alipoulizwa hajisikii vibaya kucheza na mke wa mtu alijibu kwa kifupi sana: “Kwanza ningejuaje?”

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.