Skip to main content

Zanzibar inahitaji kulinda mafanikio yaliyopatikana kutokomeza Malaria


Na Hassan Hamad OMKR
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesema Zanzibar inahitaji kujipanga ili kulinda mafanikio yaliyopatikana kutokana na mradi wa kutokomeza malaria Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na watendaji wa kitengo cha malaria Mwanakwerekwe wakati wa ziara yake katika kitengo hicho. Kushoto ni msaidizi meneja wa kitengo cha Malaria Zanzibar Bw. Mwinyi Msellem. (picha, Salmin Said, OMKR)
Amesema mafanikio yalipatikana yameiletea sifa kubwa Zanzibar, hali inayopelekea kuigwa na nchi nyengine duniani.
Maalim Seif ameeleza hayo katika kitengo cha kudhibiti malaria Zanzibar huko Mwanakwerekwe, akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya kwa upande wa Unguja.
Amesema mafanikio hayo yanapaswa kulindwa na kuhakikisha kuwa malengo yaliyotarajiwa ya kuifanya Zanzibar bila ya kuwa na Malaria yanafikiwa kwa wakati.
“Nataka hapa tulipofika tusirudi nyuma, serikali kwa upande wake itajitahidi kuweka mikakati ili kuona kuona kuwa tunasonga mbele hadi kutimiza malengo yetu”, alisistiza Maalim Seif.
Kwa upande wake msaidizi meneja wa kitengo cha Malaria Zanzibar Bw. Mwinyi Msellem amesema Zanzibar imepata mafanikio makubwa ya kupambana na malaria katika kipindi cha miaka kumi iliyopita ambapo kwa sasa ugonjwa huo upo chini ya asilimia moja kutoka asilimia 45 mwaka 2001.
Amesema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na mchango mkubwa wa washirika wa maendeleo, pamoja na mipango imara ya taasisi hiyo ikiwemo ugawaji wa vyandarua vyenye dawa, utiaji wa dawa za kuulia mbu wa malaria majumbani pamoja kufuatilia kwa karibu wagonjwa wanaougua malaria ili kuwapatia matibabu yanayostahiki.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.