Skip to main content

TIGO YA KWANZA KUTOA VIFAA VYA NISHATI YA JUA KWA AJILI YA KUCHAJIA SIMU

Tanzania ina idadi kubwa ya watu ambao hawana njia ya moja kwa moja ya kupata umeme, wakati asilimia 50 ya watanzania wanamiliki simu za mkononi. Ili kuchaji simu zao inawalazimu kwenda kwa watu wao wa karibu kama vile ndugu, jamaa, marafiki au wakati mwingine kwenye vibanda na madukani.

Ofisa Masoko wa kampuni ya Tigo Jacqeuline Nnunduma (kushoto) na Meneja Mradi wa Kampuni hiyo, Yaya N'dojere pamoja na Ofisa Uhusiano Msaidizi wa Tigo, Mariamu Mlangwa wakionesha kifaa cha solar kinavyoweza kufanya kazi ya kuchajishia simu kwa njia ya nishati ya jua.

Kwa vile asilimia kubwa ya watu hawa ni wateja wa Tigo, tumeamua kuyapa maduka yetu vifaaa vya nishati ya jua vyenye uwezo wa kuchaji simu. Kwa njia hii mteja wa Tigo kamwe hatakuwa na tatizo la simu yake kuishiwa chaji kwa ajili ya kukosa umeme.

Kwa wateja wa Tigo ambao wanaishi mbali na vyanzo vya umeme, huduma hii bunifu inarahisisha na kufanya upatikanaji wa bidhaa za Tigo uwe rahisi, pamoja na kuwapa wateja nishati rafiki na endelevu, kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku .

Kwa kupitia vifaa vya nishati ya jua ambavyo vitakuwa vikipatikana katika maduka ya Tigo, Tigo inaendelea kuwajali wateja wake ambao wanaendesha maisha na hata biashara zao katika maeneo yasiyo na umeme. Wateja watalipia kiasi nafuu cha shilingi 300 kila watakapohitaji kuchaji simu zao.

Kwa wamiliki wa maduka hayo ya Tigo, Tigo inatoa huduma za teknolojia mpya katika soko la Tanzania ili kuwasaidia wajasiriamali kupanua biashara zao na halikadhalika inaongeza kipato chao.

Wanaohitaji kujisajili kwa ajili ya vifaa wanaweza kutuma barua pepe solar@tigo.co.tz. Kigezo kinachohitajika ni kutokuwepo kwa umeme kwenye eneo husika au muhusika awe anauza chaji za simu.

Comments