Skip to main content

CAF: orodha fupi ya wachezaji bora soka


CAF
Wachezaji bora zaidi wa soka barani Afrika watatangazwa na CAF tarehe 20 Desemba
CAF imetangaza orodha fupi ya majina ya wachezaji ambao wamo katika nafasi nzuri zaidi ya kutwaa tuzo ya mchezaji bora zaidi barani Afrika.
Mshindi wa mwaka jana, Yaya Toure, anaongoza katika orodha hiyo yenye majina ya wachezaji 10, waliochaguliwa kutoka orodha ndefu ya wachezaji 34.

Mchezaji huyo kutoka Ivory Coast, ambaye ni kiungo cha kati wa timu ya Manchester City, ni kati ya wachezaji wanne wanaozichezea timu za Uingereza ambao huenda wakapata tuzo hiyo ya mwaka 2012.

Kiungo cha kati wa Chelsea, John Obi Mikel, mshambulizi wa Arsenal, Gervinho, Demba Ba wa timu ya Newcastle, ni kati ya wachezaji wengine wa ligi kuu ya Premier ambao wanawania tuzo hiyo.

Katika orodha hiyo, kuna wachezaji wengine ambao waliwahi kucheza Uingereza mwaka 2012.

Wachezaji hao ni aliyekuwa kiungo cha kati wa Arsenal, Alexandre Song, na ambaye sasa huichezea Barcelona ya Uhispania, na mshambulizi wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, ambaye anaichezea klabu ya China, Shanghai Shenhua.

Chris Katongo ni mchezaji wa pekee kutoka timu ya Zambia iliyoibuka mshindi katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Mchezaji wa Morocco, Younes Belhanda, yumo katika orodha hiyo, kwa juhudi zake mapema mwaka huu, katika timu ya Ufaransa ya daraja ya kwanza, Montpellier.

Wanaowania tuzo hiyo, watapunguzwa hadi kufikia watatu, katika wiki ya mwisho ya mwezi Novemba.

CAF vilevile ilitangaza orodha fupi ya wachezaji watano, ambao wana nafasi ya kupata tuzo la mchezaji bora barani Afrika, kwa wachezaji ambao hucheza kandanda yao barani Afrika.

Katika ordha hiyo ni pamoja na Mohamed Aboutrika, kiungo cha kati kutoka Misri, na aliyecheza katika mechi ya Al Ahly ya klabu bingwa dhidi ya Esperance ya Tunisia, mchezo uliokwishwa kwa sare ya 1-1 siku ya Jumapili.

Tuzo hizo, ambazo zitakuwa pia ni kumpa zawadi kocha bora zaidi wa mwaka, na klabu bora zaidi mwaka 2012, zitatolewa kwa washindi tarehe 20 mwezi Desemba, katika ukumbi wa Banquet, katika ikulu ya rais, katika mji mkuu wa Ghana, Accra.Source BBC swahili.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.