Uhuru Kenyatta ni mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada
ya uchaguzi mwaka 2007
Washukiwa wawili wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini
Kenya, Uhuru Kenyatta na William Ruto wanajadiliana kwa lengo la kuunda muungano
wa kisiasa watakaotumia kugombea uongozi wa nchi.
Taarifa za awali zilisema kuwa wawili hao tayari wameunda muungano huo ingawa
baadaye afisa wa mawasiliano wavigogo hao alikana kuwepo makubaliano yoyote. Wawili hao ambao ni mahasimu wa jadi kisiasa,wanaanda mkutano wa pamoja siku
ya Jumamosi mjini Nakuru mojawapo ya maeneo yaliyokumbwa na ghasia mbaya zaidi
za kikabila baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007. Na hataua ya wawili hawa inakuja wakati mahakama ikitarajiwa kutoa uamuzi
kuhusu ikiwa wanaweza kugombea uongozi wakati wanakbiliwa na tuhuma za
kuhusikana ghasia za baada ya uchaguzi ambapo mamia ya watu waliuawa. Wanasema wameamua kuunda muungano watakaoutumia kuwania nafasi ya rais na
makamu wake katika uchaguzi mkuu mwaka ujao kama ishara ya kuwapatanisha
wakenya.
Comments