Skip to main content

GAZETI LA IJUMAA : MISS TANZANIA 2012 AIBU, VITUKO!



Musa Mateja na Shakoor Jongo
KAMA uliapa kwamba Miss Tanzania 2012 itakula za uso kutokana na kiingilio kikubwa kilichowekwa, imekula kwako kwani Watanzania hususan wana-Dar es Salaam, walijaa ukumbini, hivyo kutoa uthibitisho kwamba kwao laki (Tsh. 100,000) siyo pesa kabisa.
Miss Tanzania 2012-2013, Brigitte Alfred akiwa katika pozi baada ya kutwaa taji hilo.
Katika fainali hiyo, iliyochukua nafasi kwenye Ukumbi wa Cristal, uliopo kwenye Hotel ya Blue Pearl, Ubungo Plaza, Dar, pamoja na matukio ya aibu na vituko, ilishuhudiwa kwa mtoto mkali kutoka Kitongoji cha Sinza na baadaye Kanda ya Kinondoni, Brigitte Alfred, akibeba taji la Miss Tanzania 2012-2013.
Ushindi wa Brigitte, umerudisha heshima Kinondoni baada ya kuota mbawa kwa takriban miaka minne mfululizo, kwani aliyekuwa mrembo wa mwisho kushinda taji hilo akitokea kanda hiyo ni Richa Adhia mwaka 2007.
Kino ilitisha mno kati ya mwaka 2004 hadi 2007, kwani mara zote hizo ilishinda kupitia Faraja Kotta (2004), Nancy Sumary (2005), Wema Sepetu (2006) kabla ya Richa.
AIBU ZILIZOJIRI
Mrembo aliyeshinda taji (Brigitte), alitoka ukumbini chukuchuku, baada ya Mkurugenzi wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga ‘Anko’, kusahau ‘crown’ nyumbani kwake.
Miss Tanzania 2012-2013, Brigitte Alfred (katikati) akikabidhiwa ufunguo wa gari, kulia ni Mkurugenzi wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga ‘Anko’.
Ilibainishwa kuwa katika harakati za kuwahi ukumbini, Anko alisahau mfuko wenye taji (crown) chumbani kwake na alikumbuka muda mfupi kabla ya mshindi kutangazwa, kwa hiyo alikosa namna ya kukwepa aibu hiyo.
Anko, alimnong’oneza mwandishi wetu: “Dah nimesahau crown nyumbani, sijui itakuwaje?” wakati huo shindano lilikuwa limefika hatua ya nusu fainali (15 Bora).
Brigitte amekuwa mrembo wa kwanza kutangazwa mshindi bila kuvalishwa taji.
Ukumbi wa Cristal ni mdogo, hivyo ulishindwa kutosheleza idadi ya watu, matokeo yake ulijaa mno, hivyo kusababisha joto lililosababisha kero kwa wahudhuriaji.
Miss Tanzania 2012 ilikuwa ni shoo ya VIP lakini mambo yalikwenda ndivyo sivyo, kwani pamoja na watu kulipa Tsh. 100,000 kwa kichwa, wengi walisimama, kwa hiyo hawakufaidi laki zao.
Miss Tanzania 2011-2012, Salha Israel, alipopanda kukabidhi taji, alikuwa amepooza, utadhani alilazimishwa.
VITUKO VILIKUWEPO
Kwa mwendo wa kiingilio hicho, ilidhaniwa kila anayeingia ukumbini angekuwa na usafiri wake binafsi au wa kukodi lakini haikuwa hivyo, baada ya shoo kumalizika, watu kibao walijisogeza kwenye kituo cha daladala kwa ajili ya ‘kujisevia’ usafiri wa shilingi 300.
Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, akiwa MC wa shughuli, alishindwa kuficha hisia zake kwa mwanamuziki, Nasibu Abdul ‘Diamond’, pale alipomtambulisha kama ‘Sukari ya Warembo’.
Siyo habari mpya kwamba Diamond alishawahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Jokate, kwa hiyo kitendo cha kumtambulisha hivyo kiliibua minong’ono kuwa Kidoti anamkubali ‘janki’ huyo kuwa ana ladha tamu kama sukari.
Mwanamitindo wa kiume (jina tunalo), alitolewa nishai backstage na mrembo mmoja (jina tunalihifadhi), alipokwenda kumuomba namba ya simu. Baadaye ilibainika kuwa mwanamitindo huyo alitumwa na pedeshee fulani kuchukua namba ili aanze mikakati ya kung’oa.
MENGINEYO
MOSI: Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’, alizua minong’ono, baada ya kuandika kwenye akaunti yake ya Twitter kuwa hatakwenda kwenye shoo ya fainali kwa sababu mshindi anamjua na ni mshiriki namba 26.
Matokeo ya mwisho yalipotangazwa ukumbini, FA alipatia kwa asilimia 100, kwani mrembo namba 26 ndiye Brigitte.
PILI: Warembo walioshiriki Miss Tanzania mwaka jana na miaka iliyopita, walikuwa wakizungumza huku wakisindikiza mazungumzo yao kwa vicheko kwamba huu ni muda wao kupumzika, kwani mapedeshee watawapa kisogo na kuwafuata warembo wapya, wao wakiita ‘mali mpya’.
TATU: Miss Kinondoni, ilificha nafasi zote mbili za juu, baada ya Miss Sinza, Eugine Fabian kuibuka namba mbili, wakati Miss Temeke, Eda Sylvester akiambulia namba tatu. Warembo Magdalena Loi na Happines Daniel, walikamilisha Tano Bora.
NNE: Diamond pamoja na kuingia kwa mbwembwe, alipwaya jukwaani kiasi cha kusababisha shoo yake izorote kinyume na matarajio ya wengi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.