Skip to main content

Majadiliano ya bajeti yakwama




ARCHIV - Arbeiter demontieren in der Nacht von Donnerstag (16.08.2012) am Flughafen in Frankfurt am Main eine Euro-Skulptur am Terminal. Die Verhandlungen über den EU-Haushalt des kommenden Jahres sind am Freitagabend in Brüssel gescheitert. Dies teilte ein Sprecher der EU-Kommission mit. Die Vertreter der 27 EU-Regierungen und des Europaparlamentes trennten sich ergebnislos. Foto: Fredrik von Erichsen dpa/lhe +++(c) dpa - Bildfunk+++
Juhudi za mwanzo za kupatikana makubaliano juu ya bajeti ya mwaka 2013 ya umoja wa Ulaya zimeshindwa.
Serikali za mataifa ya umoja huo pamoja na bunge zimeshindwa kupata msimamo wa pamoja kuhusu suala la utendaji baada ya karibu saa nane za mazungumzo jana Ijumaa(09.11.2012).
Pande hizo mbili zitajaribu tena kupata makubaliano siku ya Jumanne, kabla ya muda wa mwisho ambao ni usiku wa manane , kuweza kukubaliana juu ya bajeti ama kuirejesha halmashauri ya Ulaya , katika kazi ya kuipanga upya bajeti hiyo.
Wanasiasa wa umoja wa Ulaya hawatilii manani sana uchelewesho huo, na wana matumaini kuwa muda wa mwisho unaweza kufikiwa.
Jumanne ndio mwisho
"Ni pale tu ambapo hatutaweza kufanikiwa siku ya Jumanne, tuwe watulivu na hatupaswi kujiuliza kuhusu nia njema ya wadau wote," amesema Adreas Mavroyiannis, naibu waziri anayehusika na masuala ya ulaya kutoka Cyprus, nchi ambayo kwa sasa inashikilia urais wa kupokezana wa umoja wa Ulaya.
"Inatokea katika wakati wa muafaka kuwa kuna kuwa na hali ya mkwamo , wasi wasi," amesema kamishna wa bajeti ya umoja wa ulaya Janusz Lewandowski. "lakini nafikiri hali ya uwajibikaji ipo."
Mavroyiannis, hata hivyo , amesema kuwa hali ya kuweza kushindwa siku ya Jumanne "haiwezi kuondolewa kabisa".

Comments