Skip to main content

JP MPIANA KUPIGA TAFU MASHUJAA NOVEMBA 30 MWAKA HUU



Mkurugenzi wa kampuni ya QS, Mhonda Entertainment, Josefh B. Mhonda (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya ujio wa JB Mpiana.. Kulia ni Rais wa bendi ya Mashujaa, Chalz Baba.
Mshauri wa bendi ya Mashujaa, King Dodo akiongea na waandishi wa habari..
Meneja wa JB Mpiana, Guyguy Kiangala,akielezea ujio wa mwanamuziki huyo kuja kufanya onyesho hapa Tanzania.
Chalz Baba akijigamba kufanya onyesho la nguvu siku hiyo.
Waandaaji wakijinadi kwa waandishi wa habari.
KAMPUNI  ya QS ya jijini inatarajia kumleta nchini  mwanamuziki  nguli  wa  Jahmuri ya Kidemokrais ya Congo, JB Mpiana wa bendi ya Wenge BCBG katika uzindizi wa  bendi ya Mashujaa Musica ya jijini unaotarajia kufanyika katika viwanja vya Leaders  November 30 mwaka huu.
Bendi hiyo ya Mashujaa inatarajiwa kuzindua albam yao ya ‘Risasi Kidole’ yenye nyimbo sita.  Burudani zingine zitakazokuwepo siku hiyo ni  wanamuziki wa kizazi kipya ambao ni H. Baba, Ney wa Mitego, Mb Dog na wasanii wengine kibao wa muziki wa kizazi kipya.
                                                       (PICHA ZOTE NA  ISSA MNALLY/GPL)

Comments