Skip to main content

Simba itamkosa nahodha wake John Bocco Djibout


VINARA wa soka Tanzania Bara, Simba wameondoka nchini jana jioni kwenda Djibouti, kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gendarmerie Nationale utakaofanyika Februari 21.

Katika mchezo huo, Simba itamkosa nahodha wake John Bocco ambaye alifunga mabao mawili katika mchezo wa kwanza uliomalizika kwa ushindi wa 4-0, kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu wa kushoto aliyoyapata kwenye mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Mwadui FC ambapo alishindwa kuendelea na mchezo na kutolewa nje.
Akizungumza na gazeti hili Kocha Mkuu wa timu hiyo, Pierre Lechantre, alisema pamoja na kumkosa Bocco, lakini ana matumaini makubwa ya ushindi kutokana na maandalizi waliyofanya pamoja na ari waliyokuwa nayo wachezaji wake.
"Maandalizi yamekamilika, tumejipanga kuhakikisha tunacheza kwa nguvu bila kujali kama tunaongoza kwa mabao manne najua mchezo utakuwa mgumu, lakini lazima tusonge mbele kutokana na ubora wa timu yangu,” alisema Lechantre.
Mfaransa huyo alisema amesafiri na kikosi cha wachezaji 19 wenye uhakika wa kucheza na wa 20 ni Bocco ambaye ameamua kwenda naye ili kuendelea kuangalia maendeleo yake kama anaweza kuwa fiti siku ya mchezo Jumatano.
Kocha huyo ambaye amekabidhiwa kikosi cha Simba siku chache zilizopita ameoneshwa kudhamiria ushindi kutokana na ahadi ambayo ameitoa kwa viongozi na mashabiki wa timu hiyo siku aliposaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo.
Simba itashuka kwenye dimba la Stade du Ville, ambalo linabeba watazamaji 40,000 na kocha huyo amepanga kuwaanzisha washambuliaji wake wote wawili Emmanuel Okwi na Nicholaus Gyan baada ya Laudit Mavugo kubaki Dar es Salaam kutokana na kuwa majeruhi.
Wachezaji waliosafiri na kikosi cha Simba Makipa ni Aishi Salum Manula na Emanuel Elias Mseja. Mabeki Mohamed Hussein, Erasto Edward Nyoni, Shomari Kapombe, Ally Shomary, Yusufu Mlipili, Murshid Juuko na Kwasi Asante.
Viungo ni Mzamiru Yassin, Bukaba Paul, Shiza Kichuya, James Kotei, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, na Jonas Mkude.
Washambuliaji ni Emmanuel Okwi, Moses Kitandu, Nicholas Gyan na John Raphael Bocco.
Simba inahitaji sare au ushindi ili kusonga mbele raundi ya kwanza ya michuano hiyo, ambapo huenda ikakutana na Al Maasry ya Misri baada ya timu hiyo kupata ushindi wa mabao 4-0, dhidi ya Green Buffalo ya Zambia kwenye mchezo wa kwanza.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...