Skip to main content

Simba itamkosa nahodha wake John Bocco Djibout


VINARA wa soka Tanzania Bara, Simba wameondoka nchini jana jioni kwenda Djibouti, kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gendarmerie Nationale utakaofanyika Februari 21.

Katika mchezo huo, Simba itamkosa nahodha wake John Bocco ambaye alifunga mabao mawili katika mchezo wa kwanza uliomalizika kwa ushindi wa 4-0, kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu wa kushoto aliyoyapata kwenye mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Mwadui FC ambapo alishindwa kuendelea na mchezo na kutolewa nje.
Akizungumza na gazeti hili Kocha Mkuu wa timu hiyo, Pierre Lechantre, alisema pamoja na kumkosa Bocco, lakini ana matumaini makubwa ya ushindi kutokana na maandalizi waliyofanya pamoja na ari waliyokuwa nayo wachezaji wake.
"Maandalizi yamekamilika, tumejipanga kuhakikisha tunacheza kwa nguvu bila kujali kama tunaongoza kwa mabao manne najua mchezo utakuwa mgumu, lakini lazima tusonge mbele kutokana na ubora wa timu yangu,” alisema Lechantre.
Mfaransa huyo alisema amesafiri na kikosi cha wachezaji 19 wenye uhakika wa kucheza na wa 20 ni Bocco ambaye ameamua kwenda naye ili kuendelea kuangalia maendeleo yake kama anaweza kuwa fiti siku ya mchezo Jumatano.
Kocha huyo ambaye amekabidhiwa kikosi cha Simba siku chache zilizopita ameoneshwa kudhamiria ushindi kutokana na ahadi ambayo ameitoa kwa viongozi na mashabiki wa timu hiyo siku aliposaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo.
Simba itashuka kwenye dimba la Stade du Ville, ambalo linabeba watazamaji 40,000 na kocha huyo amepanga kuwaanzisha washambuliaji wake wote wawili Emmanuel Okwi na Nicholaus Gyan baada ya Laudit Mavugo kubaki Dar es Salaam kutokana na kuwa majeruhi.
Wachezaji waliosafiri na kikosi cha Simba Makipa ni Aishi Salum Manula na Emanuel Elias Mseja. Mabeki Mohamed Hussein, Erasto Edward Nyoni, Shomari Kapombe, Ally Shomary, Yusufu Mlipili, Murshid Juuko na Kwasi Asante.
Viungo ni Mzamiru Yassin, Bukaba Paul, Shiza Kichuya, James Kotei, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, na Jonas Mkude.
Washambuliaji ni Emmanuel Okwi, Moses Kitandu, Nicholas Gyan na John Raphael Bocco.
Simba inahitaji sare au ushindi ili kusonga mbele raundi ya kwanza ya michuano hiyo, ambapo huenda ikakutana na Al Maasry ya Misri baada ya timu hiyo kupata ushindi wa mabao 4-0, dhidi ya Green Buffalo ya Zambia kwenye mchezo wa kwanza.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. SÅ‚awomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...