Skip to main content

Simba itamkosa nahodha wake John Bocco Djibout


VINARA wa soka Tanzania Bara, Simba wameondoka nchini jana jioni kwenda Djibouti, kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gendarmerie Nationale utakaofanyika Februari 21.

Katika mchezo huo, Simba itamkosa nahodha wake John Bocco ambaye alifunga mabao mawili katika mchezo wa kwanza uliomalizika kwa ushindi wa 4-0, kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu wa kushoto aliyoyapata kwenye mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Mwadui FC ambapo alishindwa kuendelea na mchezo na kutolewa nje.
Akizungumza na gazeti hili Kocha Mkuu wa timu hiyo, Pierre Lechantre, alisema pamoja na kumkosa Bocco, lakini ana matumaini makubwa ya ushindi kutokana na maandalizi waliyofanya pamoja na ari waliyokuwa nayo wachezaji wake.
"Maandalizi yamekamilika, tumejipanga kuhakikisha tunacheza kwa nguvu bila kujali kama tunaongoza kwa mabao manne najua mchezo utakuwa mgumu, lakini lazima tusonge mbele kutokana na ubora wa timu yangu,” alisema Lechantre.
Mfaransa huyo alisema amesafiri na kikosi cha wachezaji 19 wenye uhakika wa kucheza na wa 20 ni Bocco ambaye ameamua kwenda naye ili kuendelea kuangalia maendeleo yake kama anaweza kuwa fiti siku ya mchezo Jumatano.
Kocha huyo ambaye amekabidhiwa kikosi cha Simba siku chache zilizopita ameoneshwa kudhamiria ushindi kutokana na ahadi ambayo ameitoa kwa viongozi na mashabiki wa timu hiyo siku aliposaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo.
Simba itashuka kwenye dimba la Stade du Ville, ambalo linabeba watazamaji 40,000 na kocha huyo amepanga kuwaanzisha washambuliaji wake wote wawili Emmanuel Okwi na Nicholaus Gyan baada ya Laudit Mavugo kubaki Dar es Salaam kutokana na kuwa majeruhi.
Wachezaji waliosafiri na kikosi cha Simba Makipa ni Aishi Salum Manula na Emanuel Elias Mseja. Mabeki Mohamed Hussein, Erasto Edward Nyoni, Shomari Kapombe, Ally Shomary, Yusufu Mlipili, Murshid Juuko na Kwasi Asante.
Viungo ni Mzamiru Yassin, Bukaba Paul, Shiza Kichuya, James Kotei, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, na Jonas Mkude.
Washambuliaji ni Emmanuel Okwi, Moses Kitandu, Nicholas Gyan na John Raphael Bocco.
Simba inahitaji sare au ushindi ili kusonga mbele raundi ya kwanza ya michuano hiyo, ambapo huenda ikakutana na Al Maasry ya Misri baada ya timu hiyo kupata ushindi wa mabao 4-0, dhidi ya Green Buffalo ya Zambia kwenye mchezo wa kwanza.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.