Skip to main content

IYF: Imezindua mpango wa ajira kwa vijana nje ya nchi


Taasisi  isiyokuwa ya Kiserikali ya Kimataifa ya Ushirika wa Vijana(IYF) ,imezindua mpango wa ajira kwa vijana nje ya nchi.Uzinduzi huo wenye kauli mbiu Najivunia Tanzania umezinduliwa jana  Jijini Dar es Salaam.


Hayo yamesemwa  wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Nkuruma uliopo  Chuo Kikuu cha Dare es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa IYF Chung  Yang alisema lengo la mpango huo nikuunga mkono Serikali katika jitihada za kupambana na tatizo la ajira
“Hakuna asiyejua kuwa kuwa kuna shida ya ajira ,Serikali ilikuwa ikiomba sekta binafsi kuibua ajira kwa kwa vijana na sisi  tumeamua kuja na mpango huu wa ajira ya kujitolea nje ya nchi ambapo watapata uzoefu katika anga za kimataifa na uzoefu .Alisema Yang.
Yang amesema wameichagua Tanzania kutokana na ukweli usiopingika kuwa vijana wengi wakitanzania ni waadirifu na wapo tayali kujitoa hivyo wameona ni vema kuwekeza nguvu zaidi Tanzania kuliko nchi nyingine.

Pichani ni Mkuu wa IYF Chung  Yang akielezea wadau waliojitokeza katika ukumbi huo Nkuruma uliopo  Chuo Kikuu cha Dare es Salaam leo. 

Vijana hao wanaotarajiwa kwenda kufanya kazi katika nchi mbali mbali idadi yao itajulikana hivi karibuni kulingana na uhitaji wa chi husika.Vijana hao watapatiwa hati ya kusafiria,Visa,na watalipiwa usafiri nakugharamiwa mahitaji yote ya msingi kama chakula malazi, na mahitaji mengine na pesa za kujikimu wawapo nchi za nje.


Kulia ni Yang akiwa na Seong Hun Kim katika mazungumzo na wanahabari Nkuruma Hall.

Kwa mujibu wa Yang nchi kati ya 25 hadi 30 zimeonesha utayali wakuchukuwa Vijana wakitanznia kufanya kazi katika nchi mbalimbali kati ya nchi 86 ambapo IYF ina hudumu.

Kipepe rushi kilichokuwa kiki muonesha kijana wa kitanzania Velence Mkulu.


Kijana Velence Mkulu akizungumza na wanahabari leo



Kwa upande wake Mshauri wa Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Paulina Mabuga ,alisema kuwa mpango huo ni mzuri na kwa chuo Kikuu Cha Dar es Salaam umekuja wakati muafaka ,wakati ambao wahitimu wengi hawana ajira.

“Kwetu sisi ni faraja kubwa ,madhumuni ya chuo ni kuandaa wahitimu wanaolitumikia Taifa na Dunia haipendezi kuona vijana wengi hawana ajira,Hata hivyo UDSM tuna mpango kama huo ambapo tunawabakisha wanafunzi kwa ajiri ya kuwaelekeza wenzao hususani mwaka wakwanza na badaye huajiriwa.Alisema Paulina.

Mwazani Ramadhani ni miongoni mwa wanufaika wa mpango wakujitolea nje ya nchi ambapo alifanya kazi Kenya kwa miezi 3 na Korea  ya Kusini  miezi 6 anaeleza ni jinsi gani mpango huo umewasaidia.
“Kutokana na soko la ajira kuwa tete mpango huu ni mkombozi kwanza umenipatia uzoefu wa kimataifa lakini umeniongezea wigo mkubwa na ufanisi katika kazi mbali mbali ikizingatiwa wenzetu wapo mbali kimaendeleo hata kitekinolojia.

Mwazani ameongeza kuwa watu wanakuwa na mitazamo hasi kuhusu watu weupe(watu wa ughaibuni)hususani kaitika suala la ubaguzi wa rangi kwa Korea ya Kusini haikuwa hivyo wanawapenda sana waafrika.
Kwa upande wake Valence Maluku mwanafunzi wa Chuo cha Teknolojia Cha Dar es Salaam ni miongoni mwa wanufaika aliyefanya kazi Uruguai kwa mwaka mmoja anasema pamoja na kwamba nchi za Amerika ya Kusini zina ubaguzi mkubwa wa rangi lakini yeye ameshinda vita kutokana na Taasi ya IYF kuwalea vizuri hivyo hakupata shida yoyote.

“Nilikuwa nikitoa elimu kuhusu athari zitokanazo na madawa ya kulevya kwa kiasi Fulani nilifaidika ikiwemo kujifunza kispaniola na kiruguai lakini nmesafiri nchi kadhaa kama Marekani,Agentina na Brazili katika mikutano mbali mbali.Alisema Maluku
Wanufaika hao wote kwa pamoja wanazungumzia changamoto ya lugha kuwa shariti ujifunze lugha na huwalazimu kujifunza kati ya miezi mitatu hadi sita ndipo unapoelewa kwa ufasaha.
Kuhusu suala la usalama wao wamekiri kuwa hawakuwa na shida ya tatatizo la usalama kwakuwa walikuwa chini ya usimamizi mzuri na Salama.

Sifa zinazohitajika ni kijana yeyote wakitanzania kuanzia miaka 18 hadi 35 ,ambapo hupatiwa mafunzo katika makambi mbali mbali nchini ,chini ya IYF na huwa na hiari yakuchagua nchi waipendayo.
IYF hufanya kazi kwa ukaribu na ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara ya Mambo ya ndani,Wizara Ushirikiano wa Kimataifa Kikanda na  Wizara ya Tamisemi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...