Skip to main content

EL-MERREIKH SASA YAMTOSA NGASA, YASEMA HAITAKI TENA MCHEZAJI KUTOKA TANZANIA




KLABU ya El-Merreikh ya Sudan imeamua kufuta mpango wake wa kumsajili mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyesajiliwa na Simba kwa mkopo akitokea Azam.
Uamuzi huo wa El-Merreikh umekuja baada ya mchezaji huyo kutafutwa kwa simu tangu jana, lakini akawa hapatikani.
Mmoja wa viongozi wa El-Merreikh aliyekuwepo Dar es Salaam kufuatilia usajili wa Ngasa, Sheikh Idrisa ameieleza TBC 1 leo asubuhi kuwa, hawamuhitaji tena Ngasa licha ya kukubaliana na klabu za Simba na Azam kuhusu uhamisho wake.
Mbali na kutomuhitaji tena Ngasa, Sheikh Idrisa alisema wamefunga milango kwa wachezaji wote wa Tanzania kwenda kucheza soka ya kulipwa Sudan kutokana na kukerwa na kitendo cha mchezaji huyo.
Uongozi wa El-Merreikh ulikuwa umetoa siku moja kwa Ngasa, kuanzia jana awe amewasiliana nao ili waweze kumwandalia mipango ya safari ya kwenda Sudan kwa ajili ya kupima afya yake na kuangalia mazingira.
Baada ya kuona mchezaji huyo hapatikani hadi leo asubuhi, Sheikh Idrisa alisema wameamua kufuta kabisa mpango wa kumsajili kwa sababu ameonyesha kuwa sio mwanamichezo mwenye kutaka kujiendeleza kimichezo.
Alipotafutwa na TBC 1 leo asubuhi, Ngasa alisema ameamua kubadili namba yake ya simu kwa vile kuanzia sasa hataki kupigiwa simu zaidi ya yeye kuwapigia wale anaowahitaji.
Ngasa alisema pia kuwa, ameamua kufuta mpango wake wa kwenda kucheza soka ya kulipwa katika klabu ya El-Merreikh kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha malipo ya ada ya uhamisho.
Mshambuliaji huyo aliyeng'ara katika michuano ya Kombe la Chalenji, iliyomalizika wiki iliyopita nchini Uganda, alisema anataka kuendelea kuichezea Simba hadi mkataba wake wa mkopo utakapomalizika Mei mwakani.
El-Merreikh imetoa dola 100,000 kwa Simba na Azam kwa ajili ya uhamisho wa mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, ambapo kila klabu itapata dola 50,000.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Ngassa atapokea kiasi cha $75,000 kama gharama ya usajili kwa mkataba wa miaka miwili, na pia atalipwa kiasi cha $ 4,000 kama mshahara kwa kila mwezi.
Kutoweka kwa Ngasa, ambaye pia alikuwa akitafutwa na viongozi wa klabu yake ya Simba bila mafanikio, kumezusha hisia kwamba amefichwa na viongozi wa Yanga, ambayo inataka kumsajili msimu ujao.
Wasiwasi wa Ngasa kufichwa na Yanga ulikuja saa chache baada ya Simba na Azam kufikia makubaliano ya kumuuza mchezaji huyo wa klabu ya El-Merreikh ya Sudan.
Simba na Azam zilifikia makubaliano hayo jana mchana baada ya kikao cha pamoja kati yao na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema jana kuwa, viongozi wa El-Merreikh wamekuwa wakimtafuta Ngasa kwa njia ya simu tangu mchana, lakini hakuwa akipatikana na haieleweki mahali alipokuwa.
Rage alisema wana wasiwasi kuwa, mchezaji huyo huenda amefichwa na wapinzani wao wa jadi Yanga, baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba wanataka kumsajili.
Hata hivyo, Rage alisema Yanga hawana uwezo wa kumsajili Ngasa kwa sasa kwa vile mkataba wake na Simba unatarajiwa kumalizika Mei mwakani. Pia alisema Yanga haina uwezo wa kulipa ada ya uhamisho wake na mshahara wa dola 4,000 kwa mwezi.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga, Bin Kleb alipoulizwa jana, alisema hawezi kusema lolote, isipokuwa atafutwe kuanzia kesho au keshokutwa.
Bin Kleb hakuwa tayari kukubali au kukataa kuhusu klabu yake kumficha Ngasa, zaidi ya kusisitiza kuwa atafutwe katika siku hizo mbili.
Kwa upande wake, Rage aliipongeza Azam kwa uamuzi wake wa kukubali kuketi meza moja na klabu yake kwa ajili ya kufikia uamuzi wa mwisho kuhusu hatma ya mchezaji huyo.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.