Skip to main content

EL-MERREIKH SASA YAMTOSA NGASA, YASEMA HAITAKI TENA MCHEZAJI KUTOKA TANZANIA




KLABU ya El-Merreikh ya Sudan imeamua kufuta mpango wake wa kumsajili mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyesajiliwa na Simba kwa mkopo akitokea Azam.
Uamuzi huo wa El-Merreikh umekuja baada ya mchezaji huyo kutafutwa kwa simu tangu jana, lakini akawa hapatikani.
Mmoja wa viongozi wa El-Merreikh aliyekuwepo Dar es Salaam kufuatilia usajili wa Ngasa, Sheikh Idrisa ameieleza TBC 1 leo asubuhi kuwa, hawamuhitaji tena Ngasa licha ya kukubaliana na klabu za Simba na Azam kuhusu uhamisho wake.
Mbali na kutomuhitaji tena Ngasa, Sheikh Idrisa alisema wamefunga milango kwa wachezaji wote wa Tanzania kwenda kucheza soka ya kulipwa Sudan kutokana na kukerwa na kitendo cha mchezaji huyo.
Uongozi wa El-Merreikh ulikuwa umetoa siku moja kwa Ngasa, kuanzia jana awe amewasiliana nao ili waweze kumwandalia mipango ya safari ya kwenda Sudan kwa ajili ya kupima afya yake na kuangalia mazingira.
Baada ya kuona mchezaji huyo hapatikani hadi leo asubuhi, Sheikh Idrisa alisema wameamua kufuta kabisa mpango wa kumsajili kwa sababu ameonyesha kuwa sio mwanamichezo mwenye kutaka kujiendeleza kimichezo.
Alipotafutwa na TBC 1 leo asubuhi, Ngasa alisema ameamua kubadili namba yake ya simu kwa vile kuanzia sasa hataki kupigiwa simu zaidi ya yeye kuwapigia wale anaowahitaji.
Ngasa alisema pia kuwa, ameamua kufuta mpango wake wa kwenda kucheza soka ya kulipwa katika klabu ya El-Merreikh kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha malipo ya ada ya uhamisho.
Mshambuliaji huyo aliyeng'ara katika michuano ya Kombe la Chalenji, iliyomalizika wiki iliyopita nchini Uganda, alisema anataka kuendelea kuichezea Simba hadi mkataba wake wa mkopo utakapomalizika Mei mwakani.
El-Merreikh imetoa dola 100,000 kwa Simba na Azam kwa ajili ya uhamisho wa mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, ambapo kila klabu itapata dola 50,000.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Ngassa atapokea kiasi cha $75,000 kama gharama ya usajili kwa mkataba wa miaka miwili, na pia atalipwa kiasi cha $ 4,000 kama mshahara kwa kila mwezi.
Kutoweka kwa Ngasa, ambaye pia alikuwa akitafutwa na viongozi wa klabu yake ya Simba bila mafanikio, kumezusha hisia kwamba amefichwa na viongozi wa Yanga, ambayo inataka kumsajili msimu ujao.
Wasiwasi wa Ngasa kufichwa na Yanga ulikuja saa chache baada ya Simba na Azam kufikia makubaliano ya kumuuza mchezaji huyo wa klabu ya El-Merreikh ya Sudan.
Simba na Azam zilifikia makubaliano hayo jana mchana baada ya kikao cha pamoja kati yao na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema jana kuwa, viongozi wa El-Merreikh wamekuwa wakimtafuta Ngasa kwa njia ya simu tangu mchana, lakini hakuwa akipatikana na haieleweki mahali alipokuwa.
Rage alisema wana wasiwasi kuwa, mchezaji huyo huenda amefichwa na wapinzani wao wa jadi Yanga, baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba wanataka kumsajili.
Hata hivyo, Rage alisema Yanga hawana uwezo wa kumsajili Ngasa kwa sasa kwa vile mkataba wake na Simba unatarajiwa kumalizika Mei mwakani. Pia alisema Yanga haina uwezo wa kulipa ada ya uhamisho wake na mshahara wa dola 4,000 kwa mwezi.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga, Bin Kleb alipoulizwa jana, alisema hawezi kusema lolote, isipokuwa atafutwe kuanzia kesho au keshokutwa.
Bin Kleb hakuwa tayari kukubali au kukataa kuhusu klabu yake kumficha Ngasa, zaidi ya kusisitiza kuwa atafutwe katika siku hizo mbili.
Kwa upande wake, Rage aliipongeza Azam kwa uamuzi wake wa kukubali kuketi meza moja na klabu yake kwa ajili ya kufikia uamuzi wa mwisho kuhusu hatma ya mchezaji huyo.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...