Skip to main content

Arsenal yaadhibiwa na Bradford

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema wachezaji wa klabu hiyo hawapaswi kuabika kufuatia kuondplewa kwao kwenye michuano ya kuwania kombe la ligi, na klabu ya Bradford inayoshiriki ligi daraja ya pili.
Arsenal iliondolewa kwenye mashindano hayo kwa kulazwa magoli 3-2 kupitia mikwaju ya penalti.
Baada ya dakika 90 za kawaida kumalizika katika uwanja wa Croal Windows, timu hizo mbili zilitoshana nguvu ya kufungana bao moja kwa moja.
Akiongea na waandishi wa habaro baada ya mechi hiyo Wenger alisema'' tulifanya kila kitu katika dakika mia moja ishirini za mechi hiyo, na bila shaka timu ya Bradford ilicheza mchezo mzuri na walistahili kushinda''
''Kwa kawaida ni jambo la aibu ikiwa hautacheza kadri ya uwezo wako, nafikiria wachezaji wangu wamehuzunishwa na matokeo hayo'' aliongeza Wenger.
Wenger alichagua kikosi kilichojumisha wachezaji wake bora wakati wa mechi hiyo, lakini hawakufanikiwa kuandikisha matokeo ya kuridhisha, na walihitaji bao dakika ya 88, bao lililofungwa na Thomas Vermaelen ili kulazimisha mechi hiyo kwenda katika muda wa ziada na hatimaye kuamiliwa kupitia mikwaju ya penalti.
Garry Thompson ndiye aliyeifungia Bradford bsao lake la kwaza katika kipindi cha kwanza.
Na kama desturi yake Wenger, alipuuzilia mbali shutuma dhidi ya wachezaji wake , ambao wameshinda mechi moja tu kati ya mechi sita walizocheza katika mashindano yote.Source. www.bbc.co.uk

Comments