Umoja wa mataifa hii leo umeanza kupeleka wanajeshi wake nchini
Mali na kufikisha idadi ya wanajeshi wanaoshika doria nchini humo na ambao
watakuwa chini ya UN hadi, 6,000.
Idadi ya wanajeshi inatarajiwa kufika 12,640 mwisoni mwa Disemba. Umoja wa Mataifa utachukua jukumu la kushika doria kutoka kwa jeshi la
Ufaransa ambalo lilisimamia operesheni ya kuwafurusha wapigananji wa kiisilamu
kutoka Kaskazini mwa nchi mwezi Januari. Jukumu lake la kwanza litakuwa kuhakikisha kuna usalama kabla ya uchaguzi wa
urais kufanyika tarehe 28 mwezi huu.
Comments