Skip to main content

Wanajeshi wa UN kuanza kazi Mali


Umoja wa mataifa hii leo umeanza kupeleka wanajeshi wake nchini Mali na kufikisha idadi ya wanajeshi wanaoshika doria nchini humo na ambao watakuwa chini ya UN hadi, 6,000.
Idadi ya wanajeshi inatarajiwa kufika 12,640 mwisoni mwa Disemba.
Umoja wa Mataifa utachukua jukumu la kushika doria kutoka kwa jeshi la Ufaransa ambalo lilisimamia operesheni ya kuwafurusha wapigananji wa kiisilamu kutoka Kaskazini mwa nchi mwezi Januari.

Jukumu lake la kwanza litakuwa kuhakikisha kuna usalama kabla ya uchaguzi wa urais kufanyika tarehe 28 mwezi huu.

Comments