Skip to main content

Mahakama yawatema makada Chadema




Picture
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Tabora, imesema haina uwezo wa kusikiliza kesi ya ugaidi inayowakabili makada watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Makada hao wanakabiliwa na shitaka la ugaidi, ambapo Juni 24, mwaka huu, waliachiwa huru na Mahakama ya Wilaya ya Igunga, kisha na wakakamatwa kwa tuhuma za kummwagia tindikali kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Tesha, katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, Mkoa wa Tabora, uliofanyika mwaka 2011.

Katika kesi hiyo, watuhumiwa ni Evodius Justunian (30), mkazi wa Bukoba, Oscar Kaijage, mkazi wa Shinyanga, Seif Magesa wa jijini Mwanza na Rajabu Daniel, mkazi wa Dodoma.

Watuhumiwa hao, walipokamatwa walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga, kabla ya Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo kukamatwa na kuunganishwa kwenye kesi hiyo.



Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora, Issa Magoli, alisema mahakama hiyo haina uwezo kisheria wa kusikiliza shauri hilo ambapo aliliahirisha hadi Julai 22, mwaka huu.

Kutokana na hali hiyo, Hakimu Magoli, aliwashauri mawakili wa upande wa utetezi, kuwasilisha hoja zao Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kuwa huko ndiko kunakoweza kupatiwa ufumbuzi wa kisheria wa shauri hilo.

Katika shauri hilo, washitakiwa hao walifunguliwa kesi mbili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Tabora, baada ya kesi ya awali ya kudhuru mwili kwa tindikali kufutwa na kufunguliwa kesi ya ugaidi dhidi ya makada hao wa Chadema.

Awali, katika shauri hilo yalizuka mabishano ya kisheria kati ya mawakili wa upande wa utetezi, wakiongozwa na Peter Kibata na Profesa Safari, huku upande wa Serikali ukiongozwa na Wakili Juma Masanja na Edifonce Mkandala.

Wakati wa mabishano hayo, mawakili wa upande wa utetezi waliomba Mahakama ifute kesi hiyo, kwa kile walichosema kuwa ni batili kutokana na baadhi ya vifungu vya sheria kukiukwa, huku mahakama hiyo ikiwa haina uwezo wa kuisikiliza isipokuwa Mahakama Kuu peke yake.

Mawakili hao walisema kuwa, washitakiwa walikamatwa sehemu tofauti, hivyo kesi zao zilipaswa kusikilizwa katika maeneo waliyokamatiwa badala ya kusikilizwa katika eneo moja.

Ulinzi mahakamani

Kabla ya washtakiwa hao kufikishwa mahakamani, Jeshi la Polisi mkoa hapa liliimarisha ulinzi katika eneo la mahakama ambapo ilipotimu saa 4 asubuhi, walifikishwa wakiwa katika gari la Polisi lenye namba za usajili PT 1816, huku wakiongozwa na askari wa kutuliza ghasia FFU.

Chanzo - Mtanzania
Picha Tumaini Makene

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...