Skip to main content

Mahakama yawatema makada Chadema




Picture
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Tabora, imesema haina uwezo wa kusikiliza kesi ya ugaidi inayowakabili makada watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Makada hao wanakabiliwa na shitaka la ugaidi, ambapo Juni 24, mwaka huu, waliachiwa huru na Mahakama ya Wilaya ya Igunga, kisha na wakakamatwa kwa tuhuma za kummwagia tindikali kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Tesha, katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, Mkoa wa Tabora, uliofanyika mwaka 2011.

Katika kesi hiyo, watuhumiwa ni Evodius Justunian (30), mkazi wa Bukoba, Oscar Kaijage, mkazi wa Shinyanga, Seif Magesa wa jijini Mwanza na Rajabu Daniel, mkazi wa Dodoma.

Watuhumiwa hao, walipokamatwa walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga, kabla ya Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo kukamatwa na kuunganishwa kwenye kesi hiyo.



Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora, Issa Magoli, alisema mahakama hiyo haina uwezo kisheria wa kusikiliza shauri hilo ambapo aliliahirisha hadi Julai 22, mwaka huu.

Kutokana na hali hiyo, Hakimu Magoli, aliwashauri mawakili wa upande wa utetezi, kuwasilisha hoja zao Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kuwa huko ndiko kunakoweza kupatiwa ufumbuzi wa kisheria wa shauri hilo.

Katika shauri hilo, washitakiwa hao walifunguliwa kesi mbili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Tabora, baada ya kesi ya awali ya kudhuru mwili kwa tindikali kufutwa na kufunguliwa kesi ya ugaidi dhidi ya makada hao wa Chadema.

Awali, katika shauri hilo yalizuka mabishano ya kisheria kati ya mawakili wa upande wa utetezi, wakiongozwa na Peter Kibata na Profesa Safari, huku upande wa Serikali ukiongozwa na Wakili Juma Masanja na Edifonce Mkandala.

Wakati wa mabishano hayo, mawakili wa upande wa utetezi waliomba Mahakama ifute kesi hiyo, kwa kile walichosema kuwa ni batili kutokana na baadhi ya vifungu vya sheria kukiukwa, huku mahakama hiyo ikiwa haina uwezo wa kuisikiliza isipokuwa Mahakama Kuu peke yake.

Mawakili hao walisema kuwa, washitakiwa walikamatwa sehemu tofauti, hivyo kesi zao zilipaswa kusikilizwa katika maeneo waliyokamatiwa badala ya kusikilizwa katika eneo moja.

Ulinzi mahakamani

Kabla ya washtakiwa hao kufikishwa mahakamani, Jeshi la Polisi mkoa hapa liliimarisha ulinzi katika eneo la mahakama ambapo ilipotimu saa 4 asubuhi, walifikishwa wakiwa katika gari la Polisi lenye namba za usajili PT 1816, huku wakiongozwa na askari wa kutuliza ghasia FFU.

Chanzo - Mtanzania
Picha Tumaini Makene

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.