Skip to main content

Tibaigana: Wapinzani wana haki kuandamana


Alfred Tibaigan
Katika mahojiano maalumu na gazeti la Mwananchi nyumbani kwake Buganguzi wilayani Muleba, Kamishna Tibaigana alisema suala la maandamano halikumsumbua kwa kuwa alielewa kuwa sheria inayaruhusu, hivyo alichokuwa akifanya ni kuwaita viongozi wa vyama vinavyotaka kuandamana na kufanya nao makubaliano ya namna maandamano hayo yanavyopaswa yafanywe kabla ya kuyaruhusu.
"Pengine hiyo ndiyo sababu sikuwahi kushambuliwa kwa maneno ya kejeli au matusi na wanasiasa kwa kuwa sikuwahi kuzuia maandamano yao bila sababu na hata kama kulikuwa na sababu niliwaita na kuwaeleza na tulikubaliana.
"Kikubwa ni kujenga tabia ya kuwaita viongozi wa waandamanaji na kujadiliana nao, vinginevyo wanaweza pia hata kukufikisha mahakamani wakipinga kuzuiwa maandamano yao," alisema Tibaigana ambaye alikumbana na sakata la kudai maandamano wakati akiwa Kamanda kwenye mikoa ya Tanga, Arusha na Dar es Salaam.(P.T)
"Nilikuwa nawaita viongozi nakaa nao tunakubaliana. Hata kama ningeambiwa na kiongozi gani nisitoe kibali, kama hakuna sababu za kweli, nilikataa kwa kuwa kisheria mimi ndiye nawajibika kama vyama vikishtaki. Ili uzuie maandamano unapaswa kuwa na sababu za msingi ambazo ukiwaeleza waandamanaji wanakuelewa."
Tibaigana anakumbuka jinsi CUF kilivyoandaa maandamano makubwa kushinikiza kuundwa kwa serikali ya mseto visiwani Zanzibar baada ya kutoridhishwa na matokeo ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005, lakini anasema kutokana na msimamo wake, haikuwa vigumu kwake kuruhusu jambo hilo.
"Wakati wa uongozi wangu CUF ilikuwa na nguvu sana, lakini mimi sikuwa na tatizo nao. Walipotaka kibali cha kuandamana niliwapa bila woga na tuliishi vizuri," anaeleza Tibaigana.
Vuguvugu la maandamano pia lilitanda wakati wa maandalizi ya ziara ya Rais wa zamani wa Marekani, George Bush nchini kutokana na wasomi na baadhi ya wanaharakati kutaka kufanya maandamano kupinga vitendo vya taifa hilo kubwa dhidi ya raia wa Palestina na sehemu nyingine ambako wananchi wasio na hatia walikuwa wakiuawa.
"Nilichofanya ni kukutana nao na kuwaeleza njia ambazo wangeweza kutumia katika maandamano hayo na hali ilikuwa shwari," alisema Kamanda Tibaigana.
Katika kipindi chake cha uongozi wa Polisi Dar es Salaam, Kamanda Tibaigana pia alikumbana na vurugu za kidini ambazo zilisababisha askari mmoja kupoteza maisha, lakini anasema kwa kushirikiana na wadau wengine, walijipanga na hali ikawa shwari.
Alivyomng'ang'ania Ditopile
Moja ya matukio makubwa wakati akiwa Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam ni tukio la mkuu wa zamani wa Mkoa wa Tabora, Ditopile kumuua dereva wa daladala baada ya kutokea kutoelewana barabarani, hali iliyolazimu sheria kufuata mkondo wake. Jeshi la Polisi lilitakiwa limkamate mkuu huyo na kumfikisha mahakamani.
Ditopile alituhumiwa kufanya mauaji hayo Novemba 5, 2006. Akidaiwa kumuua kwa kumpiga risasi dereva wa daladala, Hassan Mbonde. Alikamatwa na kufikishwa mahakamani, lakini alifariki dunia Aprili 20, 2008 wakati kesi yake ikiendelea.

Chanzo:Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...