Skip to main content

Soma hapa inshu za Coutinho


Ukiizumngumzia Yanga ya sasa, lazima umtaje kiungo Mbrazili,  Andrey Coutinho ambaye ni moto kwenye kikosi hicho. Coutinho amewateka mashabiki wa Yanga pamoja na wa timu pinzani kutokana na juhudi zake uwanjani ambapo mpaka sasa amecheza mechi nne za kirafiki walizoshinda dhidi ya Chipukizi bao 1-0, Shangani bao1-0, KMKM mabao 2-0 na Thika United bao 1-0 zote akafanya vizuri, hajawahi kuwaudhi watu wanaofuatilia  kiwango chake uwanjani.
Mwanaspoti limemfuatilia kwa umakini Coutinho katika mechi hizo na kugundua mambo makuu matano ambayo ndiyo anayowasumbua nayo wapinzani wa timu anazokutana nazo.
Anajua kufunga
Katika kikosi cha Mbrazili Marcio Maximo, Coutinho anachezeshwa pembeni kwenye winga ya kushoto. Pamoja na kuchezeshwa nafasi hiyo ni hatari sana   ndani ya18 kutokana na uwezo wake wa kufunga mabao tena kwenye nafasi ngumu.
Anaongoza kwa idadi ya mabao kwenye kikosi cha Yanga baada ya kufunga mabao mawili sawa na Mbrazili mwenzake, Genilson Santos ‘Jaja’. Mabao hayo, moja aliwafunga Shangani na lingine  KMKM zote za Zanzibar.
Ana nguvu za miguu na anacheza sana na kimahesabu na ni fundi katika upimaji wa lango pindi anapotaka kufunga. Ni mara chache anapopata nafasi ya kupiga shuti kisha apaishe au kuutoa nje mpira.
Mipira anayopiga langoni kama haikuwa bao, basi itaokolewa na kipa au mabeki.
Anapotafuta bao, anajua akae eneo gani na kuangalia namna gani atoe  uamuzi sahihi wa kupiga. Coutinho anapokuwa kwenye timu muda wowote anaweza kubadilisha matokeo ya timu kipaji ambacho ni viungo wachache wanacho.
Kuchezesha timu
Mbrazili huyo ni mtaalamu wa kuchezesha timu. Pasi zake fupi na ndefu, zinafika vizuri kwa mtu anayemkusudia. Ikitokea bahati mbaya mahesabu yake yamekataa na kupoteza mpira, atahakikisha anautafuta kwa kukaba hadi mwisho, si yule anayekata tamaa mapema.
Anajua kujiweka katika nafasi nzuri na sasa ana uelewano mzuri na Mnyarwanda Haruna Niyonzima  ‘Fabregas’, Mrisho Ngassa na Geilson Santos Santana ‘Jaja’ na wanatengeneza kombinesheni nzuri.
Akili na ujanja
Mhimili mkubwa wa Coutinho awapo uwanjani ni akili, ubongo wake unafanya kazi na kutoa uamuzi sahihi kwa haraka mno. Anapokuwa na mpira anajua kujipangia majukumu namna atakavyoutumia na anapokuwa hana, anaelewa namna gani afanye ili mambo yaende sawa.
Ni mjanja sana jamaa na kwa taarifa, wale jamaa zangu wenye sifa za kucheza faulo za kijinga, ukimchezea Coutinho anakuumbua. Anapenya sana uwanjani na anateleza mithili ya nyoka.
Kasi na Wepesi
Kiungo huyu hana mwili mkubwa ni saizi ya kati, lakini ni mwepesi mno, anaweza kuwa mbele anashambulia baada ya sekunde chache unaweza kumwona nyuma anazuia. Ana kasi katika kupanda na kuzuia na msumbufu sana, kama beki anayecheza naye hayuko sawa, anaumbuka.
Mguu wake wa kushoto hatari
Coutinho anatumia miguu yote kucheza, lakini ule wa kushoto ni hatari. Ndiyo siraha kubwa kwake, shuti lake linalotoka kwenye mguu huo ni zito. Mabao yake mawili, ameyafunga kwa kutumia mguu huo.
-Makala kutoka Mwanaspoti.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...