Skip to main content

Liverpool yatoka sare na Everton


Timu ya Liverpool imeendelea na kupata matokeo yasiyo mazuri katika ligi ya uingereza baada ya wiki iliyopita kupata kipigo cha mabao 3-1 dhidi ya West Ham United na leo imeweza kulazimishwa sare katika uwanja wake wa nyumbani Anfield na Everton.
Bao la nahodha Steven Gerrad dakika ya 65 lilionekana kuwapa alama zote Liverpool katika mchezo wa leo .Mchezo uliendelea kwa kasi sana na mnamo dakika za majeruhi Jagielka wa Everton kutoka umbali wa yadi 30 aliachia bunduki kali sana na kuokoa timu yake na kufanya mchezo kuishia 1-1.

Comments