Skip to main content

WEMA DIAMOND, WAKUTANISHWA KWENYE FILAMU



Waandaaji wavunja benki kuwalipa washiriki
Diamond akiri itakuwa kazi ngumu kuliko muziki

LICHA ya kuvunjika kwa uhusiano wao wa kimapenzi, msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' na msanii nyota wa filamu, Wema Sepetu watakutanishwa katika filamu.

Wapenzi hao wawili, ambao wamekuwa wakirudiana na kuachana mara kwa mara, wanatarajiwa kucheza filamu mpya itakayoanza kurekodiwa hivi karibuni.

Akihojiwa katika kipindi cha Take One Action kilichorushwa hewani hivi karibuni na kituo cha televisheni cha Clouds, Diamond alisema amelipwa pesa nyingi kwa ajili ya kucheza filamu hiyo.

Diamond alisema hakuna msanii wa filamu aliyewahi kulipwa kiwango hicho cha pesa na kwamba hata yeye hajawahi kulipwa pesa kama hizo katika kazi yake ya muziki.

Hata hivyo, Diamond hakuwa tayari kutaja kiwango hicho cha pesa kwa madai kuwa, taarifa zaidi zitatolewa na waandaaji wa filamu hiyo hivi karibuni.

"Taarifa kuhusu filamu hiyo inahusu nini, lini tutaanza kufanya 'shooting', washiriki wamelipwa kiasi gani cha pesa na picha zake zitachukuliwa maeneo gani, itatolewa na waandaaji,"alisema

Msanii huyo nguli wa muziki wa kizazi kipya alisema anaamini filamu hiyo itakuwa babu kubwa kutokana na maelezo aliyopewa na waandaaji wake.

 "Haitakuwa kama hizi filamu zilizozoeleka,"alisema msanii huyo, ambaye amewahi kushinda tuzo kadhaa za muziki za Kilimanjaro.

Diamond alisema amewahi kuombwa na watu mbalimbali kucheza filamu zao, lakini amekuwa akiwatolea nje kutokana na kutoridhishwa na maudhui yake na mazingira ya uandaaji wake.

Alisema lengo lake ni kuifanya filamu hiyo atakayoicheza kwa kushirikiana na Wema, iwe katika kiwango cha juu ili aweze kuuza jina lake kimataifa.

Licha ya kukubali kucheza filamu hiyo, Diamond alisema anahisi kutatokea matukio mengi ya ajabu wakati wa kupiga picha za filamu hiyo katika maeneo husika.

"Nina hakika baadhi ya wakati mpenzi wangu atakuwa akija kwenye maeneo ya kupiga picha za filamu hiyo kila atakapopata nafasi, hivyo kutakuwa na vijembe na maneno ya hapa na pale,"alisema.

"Hii kazi nahisi itakuwa ngumu kuliko hata ya muziki, lakini namuomba Mungu anisaidie ili niweze kuimaliza salama,"aliongeza msanii huyo.

Japokuwa hakutaka kuweka wazi kuhusu wasiwasi alionao wa kutokea matukio ya ajabu wakati wa upigaji wa picha za filamu hiyo, kauli yake hiyo inamuhusisha Wema na mpenzi wake wa sasa, Penny.

Diamond ana wasiwasi kuwa, iwapo Penny atakuwa akimtembelea katika maeneo watakayokuwa wakipiga picha za filamu hiyo, huenda akakwaruzana na Wema na kurushiana vijembe.

"Si unajua kila mtu analinda chake. Nina hakika yataripotiwa mambo mengi wakati wa kupiga picha za filamu hiyo,"alisema.

Alipoulizwa ni msanii yupi wa filamu wa kike anayevutiwa naye, Diamond hakusita kumtaja Wema.

"Napenda sana uigizaji wa Wema, si kwa sababu alikuwa mpenzi wangu. Waswahili wanasema palipo na ukweli, hakuna haja ya kuficha mambo. Wema anaigiza vizuri sana,"alisema.

Kwa upande wa wacheza filamu wa kiume, Diamond alimtaja msanii anayemvutia kuwa ni Jacob Steven, maarufu kwa jina la JB.

Diamond amewataka watanzania kujenga tabia ya kuwasamehe wasanii pale wanapoteleza na kufanya matendo mabaya mbele ya jamii. Alisema inasikitisha kuona kuwa, matendo mabaya yanavuma zaidi kuliko mazuri.

"Mimi kama Diamond nimekuwa nikifanya mambo mengi mazuri, lakini hayaonekani. Lakini inapotokea nimefanya kitu kidogo chenye mwonekano mbaya, kinakuzwa sana,"alisema.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...