Skip to main content

WEMA DIAMOND, WAKUTANISHWA KWENYE FILAMU



Waandaaji wavunja benki kuwalipa washiriki
Diamond akiri itakuwa kazi ngumu kuliko muziki

LICHA ya kuvunjika kwa uhusiano wao wa kimapenzi, msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' na msanii nyota wa filamu, Wema Sepetu watakutanishwa katika filamu.

Wapenzi hao wawili, ambao wamekuwa wakirudiana na kuachana mara kwa mara, wanatarajiwa kucheza filamu mpya itakayoanza kurekodiwa hivi karibuni.

Akihojiwa katika kipindi cha Take One Action kilichorushwa hewani hivi karibuni na kituo cha televisheni cha Clouds, Diamond alisema amelipwa pesa nyingi kwa ajili ya kucheza filamu hiyo.

Diamond alisema hakuna msanii wa filamu aliyewahi kulipwa kiwango hicho cha pesa na kwamba hata yeye hajawahi kulipwa pesa kama hizo katika kazi yake ya muziki.

Hata hivyo, Diamond hakuwa tayari kutaja kiwango hicho cha pesa kwa madai kuwa, taarifa zaidi zitatolewa na waandaaji wa filamu hiyo hivi karibuni.

"Taarifa kuhusu filamu hiyo inahusu nini, lini tutaanza kufanya 'shooting', washiriki wamelipwa kiasi gani cha pesa na picha zake zitachukuliwa maeneo gani, itatolewa na waandaaji,"alisema

Msanii huyo nguli wa muziki wa kizazi kipya alisema anaamini filamu hiyo itakuwa babu kubwa kutokana na maelezo aliyopewa na waandaaji wake.

 "Haitakuwa kama hizi filamu zilizozoeleka,"alisema msanii huyo, ambaye amewahi kushinda tuzo kadhaa za muziki za Kilimanjaro.

Diamond alisema amewahi kuombwa na watu mbalimbali kucheza filamu zao, lakini amekuwa akiwatolea nje kutokana na kutoridhishwa na maudhui yake na mazingira ya uandaaji wake.

Alisema lengo lake ni kuifanya filamu hiyo atakayoicheza kwa kushirikiana na Wema, iwe katika kiwango cha juu ili aweze kuuza jina lake kimataifa.

Licha ya kukubali kucheza filamu hiyo, Diamond alisema anahisi kutatokea matukio mengi ya ajabu wakati wa kupiga picha za filamu hiyo katika maeneo husika.

"Nina hakika baadhi ya wakati mpenzi wangu atakuwa akija kwenye maeneo ya kupiga picha za filamu hiyo kila atakapopata nafasi, hivyo kutakuwa na vijembe na maneno ya hapa na pale,"alisema.

"Hii kazi nahisi itakuwa ngumu kuliko hata ya muziki, lakini namuomba Mungu anisaidie ili niweze kuimaliza salama,"aliongeza msanii huyo.

Japokuwa hakutaka kuweka wazi kuhusu wasiwasi alionao wa kutokea matukio ya ajabu wakati wa upigaji wa picha za filamu hiyo, kauli yake hiyo inamuhusisha Wema na mpenzi wake wa sasa, Penny.

Diamond ana wasiwasi kuwa, iwapo Penny atakuwa akimtembelea katika maeneo watakayokuwa wakipiga picha za filamu hiyo, huenda akakwaruzana na Wema na kurushiana vijembe.

"Si unajua kila mtu analinda chake. Nina hakika yataripotiwa mambo mengi wakati wa kupiga picha za filamu hiyo,"alisema.

Alipoulizwa ni msanii yupi wa filamu wa kike anayevutiwa naye, Diamond hakusita kumtaja Wema.

"Napenda sana uigizaji wa Wema, si kwa sababu alikuwa mpenzi wangu. Waswahili wanasema palipo na ukweli, hakuna haja ya kuficha mambo. Wema anaigiza vizuri sana,"alisema.

Kwa upande wa wacheza filamu wa kiume, Diamond alimtaja msanii anayemvutia kuwa ni Jacob Steven, maarufu kwa jina la JB.

Diamond amewataka watanzania kujenga tabia ya kuwasamehe wasanii pale wanapoteleza na kufanya matendo mabaya mbele ya jamii. Alisema inasikitisha kuona kuwa, matendo mabaya yanavuma zaidi kuliko mazuri.

"Mimi kama Diamond nimekuwa nikifanya mambo mengi mazuri, lakini hayaonekani. Lakini inapotokea nimefanya kitu kidogo chenye mwonekano mbaya, kinakuzwa sana,"alisema.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...