Skip to main content

Msome Riyama Ally


Riyama Ally
Riyama Ally mwigizaji wa filamu Swahiliwood.
MWANADADA Mahiri katika uigizaji wa filamu Swahiliwood Riyama Ali amewashukia baadhi ya wasanii ambao ujisahau baada ya kutoka katika uigizaji wa filamu na kuwa nyota, Riyama anasema kuwa amewasaidia wasanii wengi kisanaa lakini badala yake wamegeuka maadui wala hawana hata shukrani kwake tabia hiyo anaamini ipo sana kwa wasanii wengi wachanga wakitoka.

.
Riyama ally
Riyama Ally msanii wa filamu Swahiliwood.
“Wasanii wa kike tuna tabia ya kujisahau sana katika uhusiano na ni watu wasiopenda kujulikana walikotoka, unamkutana msichana hana mbele wala nyuma, anakuja anakufuata kwa maneno matamu ooh dada nakupenda unavyoigiza natamani niwe kama wewe unaonyesha upendo na kumsaidia akicheza filamu moja tu anaanza kukunanga,”anasema Riyama.
.
Riyama Ally
Riyama Ally katika pozi.
Aidha mwanadada huyo mwenye uigizaji wa kipekee katika filamu ameenda mbali baada ya kuwashutumu waigizaji wa kike kwa kukosa kabisa upendo wa kweli na kuwa waigizaji hata katika maisha ya kawaida jambo ambalo linawafanya wadharauliwe katika jamii yao, hadi imefikia kwa msanii anayejielewa kuchukia kuitwa jina la Bongo movie.Inatoka kwa mau.

Comments