Skip to main content

Soma habari hii kutoka kwa Saleh Ally, Coruna



 
MTEMBEZI ambaye anatafuta kujifunza si sawa na aliyekaa tu nyumbani akiamini vitu vitakuja na kumfuata mahali alipo.

  Kila ninapopata safari hasa zinazohusiana na masuala ya soka au burudani, nimekuwa nikipenda kujifunza na wadau wa tasnia husika. Ninajua haitakuwa rahisi kila mmoja kupata nafasi anayoipata mwingine.
 Ikitokea mwingine akapata nyingine, basi inakuwa rahisi kushirikiana nao kwa kuwaeleza aliona nini na kujifunza kipi ili awasaidie na wengine.

 Nilipotua katika Mji wa Coruna ambao upo Kaskazini Magharibi mwa nchi ya Hispania, nimejifunza mengi likiwemo moja ambalo sikuwahi hata kulisikia.

Wakati tukiwa katika ziara ya kutembelea Uwanja wa Raizor unaomilikiwa na Derpotivo la Coruna waliokuwa wanatarajia kuwakaribisha Barcelona katika mechi ya La Liga, kesho yake, yaani juzi, niligundua jambo moja la ajabu kidogo kuhusiana na vyumba vya kubadilishia nguo.

    tJambo hilo lilifanya niamini kweli mpira ni fitna hata kama inaweza kuwa ni halali. Pia mpira ni kuwachanganya wapinzani kisaikolojia. Hivyo kujiandaa kimwili ili kuwa fiti ni sehemu moja tu, lakini saikolojia ni muhimu sana.

  Wakati tunazunguka katika vyumba vya kubadilishia nguo ndani ya uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu 43,600 tulianzia katika vyumba vya wageni. Yaani timu itakayofika pale kucheza dhidi ya wenyeji wake, Derpotivo la Coruna.

Hakika nilishangazwa kidogo, mazingira ya uwanja huo yalikuwa mazuri sana katika kila sehemu tulizopita, lakini vyumba vya timu mgeni yalionekana ni ya hovyo kabisa. Ajabu zaidi waliweka msisitizo si sahihi kupiga picha.

Basi, nikaona huenda kwa timu za Hispania, zimefeli katika kuweka mazingira mazuri vyumbani. Tukaendelea na ziara sehemu ya upande wa pili yaani kwenye vyumba vya kubadilishia nguo vya wenyeji.

Hapo nikashangazwa zaidi hadi nikaona ni wakati wa kujifunza. Hakika vyumba vilikuwa vizuri kama nilivyotarajia mwanzo.

 Sehemu nzuri kwa ajili ya masaji na matibabu kwa wachezaji. Hata vile viti vya kulaza wagonjwa na vile vya watu kwa matibabu, pia vilikuwa bora ukilinganisha na vile tulivyoviona kwa upande wa timu mgeni.

Nilipouliza, jibu kutoka kwa Armando Pelleiro wa Gazeti la DXT Compeon ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Habari na Msemaji wa Derpotivo la Coruna, lilikuwa hivi;

“Hii nenda kwenye uwanja wowote duniani, imekuwa ni utamaduni kwa vyumba vya wageni kuwa na hali ambayo si nzuri sana. Utaona hata choo kinatoa harufu kwa mbali.

“Sehemu ya kuogea pia si nzuri, mabenchi yao ni mabaya na hii tunafanya makusudi kabisa. Ukiingia Camp Nou au Santiago Bernabeu iko hivi na wenyewe wanajua.

“Mgeni ni mtu mzuri, lakini mgeni anayekuja kwako kukunyima raha na familia yako kwa kukufunga lazima uhakikishe hana raha kabla hajafanya hivyo.

“Timu zote za Hispania zinafanya hivi. Huu ni utamaduni wa soka la Hispania. Hatuwezi kwenda Camp Nou, halafu Barcelona watuweke kwenye sehemu ya hovyo halafu waje hapa sisi tuwape nafasi ya kutulia kisaikolojia,” anasema Pelleiro.

Hakika vyumba hivyo viwili vilikuwa ni vya aina tofauti utafikiri haviko katika uwanja mmoja. Nilijiuliza mara mbili kama kweli wachezaji wakubwa na maarufu kama Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar nao watakuwa kwenye vyumba hivyo juzi Jumatano.

Kumbe kumfanya adui asitulie si jambo baya katika soka ili mradi isiwe haramu na Pelleiro anasema, hakuna anayezoea shida au maisha mabaya na kila siku anapambana kuimaliza.

“Unaweza kusema timu ikipita kwenye viwanja vibaya inazoea, si kweli. Wachezaji wakubwa wanateseka sana. Unajua Lionel Messi au Cristiano Ronaldo wanaishi kwenye sehemu za kifahari. Kuwaweka kwenye vyumba vyenye hali mbaya vinawachanganya, hata kama wajikaze vipi hawawezi kuzoea.”

Umeisikia hiyo? Yanga na Simba wanaweza vipi kufanya fitina ya namna hiyo wakati wote wanaazima viwanja?

Azam FC wenyewe uwanja wao ambao tunawapongeza wanalijua hili? Au ndiyo ule mfumo wa Kitanzania wa “kumkarimu mgeni”. Tena mgeni anayekudhuru. Tujifunze.





Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...