Skip to main content

Ban ambana Machar kurejea haraka Juba

Südsudan Rebellenführer Riek Machar
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon Ijumaa (22.04.2016) amemuwekea mbinyo zaidi kiongozi wa waasi nchini Sudan kusini Riek Machar kurejea mjini Juba "bila kuchelewa" na kuanza kazi katika serikali ya mpito.
Machar alitarajiwa kurejea katika mji mkuu siku ya Jumatatu, kwa mujibu wa makubaliano ya kisiasa yenye lengo la kumaliza vita vya miaka miwili, lakini tofauti kuhusiana na mipango ya kiusalama mjini Juba inachelewesha kurejea kwake.
Ban amesema serikali ya rais Salva Kiir imekubali pendekezo la muafaka kuhusiana na matayarisho ya kurejea kwa Machar na kusema hatua hii inapaswa kusaidia kuundwa kwa haraka kwa serikali mpya ya umoja wa kitaifa.
"Kuendelea na hali ya ushirikiano itakuwa muhimu wakati viongozi wa nchi hiyo wakianza mchakato wa kubadilisha miaka ya uharibifu uliosababishwa na mzozo huo kwa watu wa Sudan kusini," amesema katika taarifa.
Mateso ya watu wa Sudan kusini
Ban amemtaka Machar kusafiri kwenda Juba " bila masharti zaidi" hali ambayo inaweza kuchafua mchakato wa amani na kuendeleza hali ya mateso yanayowakuta watu wa Sudan kusini."(P.T)
Chini ya makubaliano ya amani, Machar alitakiwa kurejea tena katrika wadhifa wake wa makamu wa rais katika serikali mpya itakayodumu kwa muda wa miezi 30 na kuielekeza nchi hiyo katika uchaguzi mkuu.
Kikwazo cha hivi sasa kinahusiana na idadi ya bunduki na vifaa vya kufyatulia maguruneti ambavyo vikosi vya waasi vinavyomlinda Machar vitaruhusiwa kuwa navyo.
Vita vya Sudan kusini vilianza Desemba mwaka 2013, wakati Kiir alipomshutumu Machar kwa kula njama za kumpindua. Mzozo huo umeweka wazi mpasuko wa tofauti za kikabila na umekuwa ukionesha ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na ubakaji wa makundi, uchomaji moto vijiji na hata ulaji nyama za watu.
Ombi la Marekani
Kwa ombi la Marekani, baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilikutana siku ya Jumatatu na kuelezea "wasi wasi wake mkubwa " kwa kushindfwa kurejea Machar mjini Juba.
Jumuiya zenye nguvu duniani, ikiwa ni pamoja na Umoja Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya , China , Uingereza na Marekani , zimewapatia Machar na Kiir muda wa mwisho hadi leo Jumamosi (23.04.2016) kutatua tofauti zao.
Mamia kwa maelfu ya watu wameuwawa na zaidi ya watu wengine milioni mbili wamelazimika kuyakimbia makaazi yao tangu vita hivyo vilipozuka Desemba mwaka 2013.
Wasiwasi unatuwama katika hali ya kutoaminiana kuhusiana na silaha hali ambayo imechelewesha kurejea kwa Machar.
Kikosi cha wanajeshi waasi wapatao 1,370 tayari kimewasili mjini Juba kama sehemu ya makubaliano ya amani wakati majeshi ya serikali yanasema yameondoa wanajeshi wake wote isipokuwa wanajeshi 3,420 , kwa mujibu wa makubaliano. Wanajeshi wengine wote wanapaswa kubakia kiasi ya kilometa 25 nje ya mji mkuu.
Katika moja kati ya kambi tatu za waasi mjini Juba, waasi wanatengana na kambi ya majeshi ya serikali kiasi ya mwendo wa miguu wa dakika tano na wanaweza kuonana na karibu iwapo kutatokea rabsha zozote.
Chanzo:DW

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.