Skip to main content

Rais Magufuli Azingumzia Watumishi Hewa




Rais John Magufuli juzi aliwazungumzia makada walioihama CCM wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliopita, alipoeleza kuwa kuondoka kwao pengine kulimsaidia kupata ushindi.


Bila kutaja majina ya waliokihama chama, Magufuli alisema ni vyema wana CCM wakasahau tofauti zilizojitokeza wakati wa uchaguzi huo na kuganga yajayo.


Rais alisema hayo kwenye mkutano na viongozi wa CCM wa mikoa na wilaya zote nchini, uliofanyika juzi Ikulu jijini Dar es Salaam.


Alisema kuna mengi yalitokea wakati wa uchaguzi huo na yalikidhoofisha chama na hivyo kuna haja ya kuyasahau yaliyopita na kuangalia mbele katika kukijenga chama.


“Lakini inawezekana wale walioamua kwenda kule walisaidia mimi kushinda,”alisema bila ya kufafanua.


Baadhi ya wana CCM waliokihama chama hicho wakati wa uchaguzi huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa kuanzia ndani ya chama hicho ni pamoja na mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowasa aliyehamia Chadema, Frederick Sumaye, ambaye kwanza alitangaza kujiunga na upinzani bila ya kutaja chama na mapema mwaka huu kukabidhiwa kadi ya Chadema.


Mwingine ni aliyekuwa kada mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale Mwiru, Balozi Juma Mwapachu, mawaziri, wabunge na madiwani, wengi wakijiunga na Chadema, ambayo ilimsimamisha Lowassa kuwa mgombea wake wa urais akiungwa mkono na vyama vya NLD, NCCR-Mageuzi na CUF vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).


Lowassa alionekana kuwa kinara kwenye harakati za urais ndani ya CCM, akichuana vikali na Bernard Membe, lakini jina lake halikufikishwa kwenye Kamati Kuu, ambayo ilitangaza majina matano, akiwamo Magufuli, yaliyopelekwa Halmashauri Kuu ya chama hicho.


Kitendo hicho kilifanya wajumbe wa Halmashauri Kuu kumpinga waziwazi mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na baada ya juhudi za wazee wa chama hicho, hali ilitulia na Magufuli akaongoza kwa kura nyingi. Baadaye Lowassa alitangaza kuhamia Chadema na kufuatiwa na wanachama kadhaa.


Alipotangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu, Magufuli alisema wakati akihutubia wanaCCM kwenye ofisi ndogo ya chama hicho Lumumba jijini, alisema uchaguzi huo ulikumbwa na hujuma zilizofanywa na wanafiki waliojificha ndani ya chama hicho.


Alisema ni vema wanafiki hao wakajisalimisha kwa kutubu kwa kuwa wamekigharimu chama hicho na kusababisha kiwe kwenye wakati mgumu.


Dk Magufuli alisema anaona ni bora kuishi na mchawi kuliko mnafiki, na kumuomba Kikwete asiwahurumie wanaokihujumu chama.


CCM walikidhoofisha chama

Juzi, akizungumza kwenye mkutano huo na viongozi wa CCM ambao katika hali isiyokuwa ya kawaida hawakuvaa sare zao za chama, Magufuli alisema waliokidhoofisha chama ni wana CCM wenyewe na ndiyo maana wapinzani walitumia udhaifu huo kukisaliti.


“Tulithamini fedha kuliko chochote. Wala hatukuuliza hizi fedha zimetoka wapi. Tuliowapa miradi, walituchezea, tumejikaanga CCM kwa mafuta yetu wenyewe. Kama tulifanya makosa, tusifanye tena,” alisema.


Aliwataka viongozi hao wa CCM kuanza kuzungukia maeneo yao ili kuwashukuru wananchi kwa ushindi na kukiimarisha chama.


“Kwa kifupi, nyinyi ndiyo Serikali. Kiongozi yeyote mnayemuona hatekelezi ilani yake, huyo hafai kwenye safari hii. Mimi niwaahidi hatutasita kuchukua hatua kwa wale mtakaoona hawafai,” alisema.


Awali Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana alisema Kamati Kuu ya CCM imepokea ripoti ya uchaguzi huo wa Oktoba 25 kutoka mikoa yote na wiki ijayo itafanyika tathmini ya maandalizi, mchakato wa kuwapata wagombea, matokeo, upigaji kura na utangazaji wa matokeo.


Azungumzia Watumishi Hewa  CCM

Kadhalika, Magufuli alimtaka Kinana kuanza kuchukua hatua za kuondoa wafanyakazi hewa ndani ya chama hicho.


“Na mimi nina uhakika katibu mkuu hata kwenye chama wapo wafanyakazi hewa kwa sababu watu ni wale wale, ni Watanzania wale wale. Kwa hiyo na wewe uanze kuchukua hatua dhidi ya wafanyakazi hewa walioko kwenye chama,” alisema.


Alisema Serikali inatumia zaidi ya Sh583 bilioni kulipa mishahara, lakini mpaka sasa kuna wafanyakazi 7,700 hewa wakati uchambuzi bado ukiendelea.Inatoka Udaku Specially

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...