Skip to main content

NWANKO KANU ATEMBELEA TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE MUHIMBILI

 

kanu1
Mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Nigeria, Super Eagles, Nwankwo Kanu ambaye pia ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akiwasili katika Jengo la Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete lililopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako amewatembelea wagonjwa wa moyo leo. Kanu atakiwepo nchini kwa muda wa siku tano kushiriki shughuli mbalimbali za kampuni na kijamii.
kanu2
Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo, Dk Peter Kisenge katika taasisi hiyo akimkaribisha Nwankwo Kanu Ambaye pia ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika. Kanu atakuwepo nchini kwa muda wa siku tano kushiriki shughuli mbalimbali za kampuni na kijamii.
kanu3
Nwankwo Kanu ambaye pia ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akimsikiliza Daktari bingwa katika Taasiai ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk Peter Kisenge wakati akitoa taarifa fupi ya taasisi hiyo
kanu4
Aliyekuwa mchezaji nyota wa timu ya taifa ya Nigeria, Nwanko Kanu akifafanua jambo kwa madaktari wa taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo hospitali ya taifa ya Muhimbili wakati alipotembelea hapo.(P.T)
kanu5
Aliyekuwa mchezaji nyota wa timu ya taifa ya Nigeria, Nwanko Kanu akimsikiliza mmoja wa madaktari wakati alipotembelea katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili leo huku madaktari wa hospitali hiyo wakifuatilia mazungumzo hayo.
kanu6
Mmoja wa wagonjwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ya hospitali ya taifa ya Muhimbili mtoto Mariam Omary akifurahi baada ya kupata fursa ya kutembelewa na kujuliwa hali na aliyekuwa mchezaji nyota wa nigeria, Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika.
kanu7
Fatuma Shaban akipokea zawadi kutoka kwa aliyekuwa mchezaji nyota wa timu ya taifa ya Nigeria na kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika Nwankwo Kanu kwa niaba ya mtoto wake, Ramadhan Shaban ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo kwenye taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika  hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
kanu8
Aliyekuwa mchezaji nyota wa timu ya Taifa ya Nigeria Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akizungumza jambo na madaktari katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) alipotembelea taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete ya hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Aliyekuwa mchezaji nguli wa timu ya taifa ya Nigeria au Super Eagles, Nwankwo Kanu ambaye pia kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika leo ametembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili (MNH) kwa lengo la kujua ni jinsi gani taasisi hiyo inafanya kazi pamoja na kuwajulia hali wagonjwa wa moyo waliolazwa katika Taasisi hiyo. pia
Akizungumza  baada ya kuwasili katika Taasisi hiyo Kanu ameelezea kuguswa na tatizo la ugonjwa wa moyo hasa kwa watoto wadogo ambao amewatembelea na kuahidi kubadilishana uzoefu kuhusu huduma za matibabu zinazotolewa na wataalamu wa tasisi hiyo.
“Tatizo la moyo ni kubwa sana kwa sasa na limekuwa likiongezeka kwa kasi lakini cha kusikitisha ni kuwa sio kila mtu anaweza kumudu gharama za matibabu yake. Hivyo basi kuna umuhimu mkubwa sana kwa serikali na wadau wengine kuanzisha vituo maalumu kama hivi ili kuwasaidia wasiojiweza.” Alisema Kanu
Katika mazungumzo yake mchezaji huyo wa nyota wa zamani ambaye aliwahi kuwika na vilabu kama vile vya Arsenal, Ajax na Inter Milan, amesema kuwa pamoja na kuja kwa shughuli mbalimbali kama balozi wa kampuni ya StarTimes lakini pia ana nia ya kushirikiana na watalaamu wa Taasisi hiyo ya Moyo. Alielezea kuwa lengo ni kuwasaidia matibabu watoto wenye matatizo ya Moyo ambao wazazi wao hawana uwezo na kwamba watazungumzia suala hilo.
“Nimefarijika sana kuona serikali ya watu wa Tanzania inachukua hatua stahiki katika kuwasaidia wananchi wake. Pia ningependa kuchukua fursa hii kuwataka watanzania hasa wanamichezo kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara kwani ukijua tatizo mapema ni rahisi kupata matibabu na kupona. Tumeona mifano michache ya wachezaji maarufu mbalimbali barani Afrika na kwingineko duniani wakifariki au kunusurika kufa wakiwa katika ya mchezo kutokana na kutoweka wazi mustakabali wa afya zao.” Alihitimisha balozi huyo wa StarTimes barani Afrika
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Upasuaji kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Dkt. Godwin Godfrey amelezea kuwa tangu Julai mwaka jana mpaka sasa tasisi hiyo kwa kushirikiana na wataalam kutoka nje ya nchi wamewafanyia upasuaji watoto zaidi ya 200.
Nwankwo Kanu mbali na kujizolea umaarufu na heshima kubwa katika medani za soka barani Afrika na Ulaya yeye pia alifanyiwa upasuaji wa moyo mwaka 1996 na ndipo alipoamua kufungua taasisi yake ya moyo inayoitwa “The Kanu Heart Foundation.”
Taasisi yake hiyo iliyoko nchini Nigeria ambako ndiko alipozaliwa aliianzisha kwa madhumuni makubwa ya kusaidia wenye matatizo kama yake na ameahidi taasisi hiyo kushirikiana na taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika masuala mbalimbali.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.