Skip to main content

KIWANGO SAFI CHA OSCAR JOSHUA DHIDI YA AL AHLY, HAJI MWINYI KAYASEMA HAYA…


 

 
Haji Mwinyi

Mlinzi wa kushoto wa Yanga Haji Mwinyi amesifia kiwango cha mlinzi mkongwe Oscar Joshua wa klabu hiyo ambaye wamekuwa wakichuana kuwania nafasi katika kikosi cha kwanza, Mwinyi kwa sasa anauguza majeraha ambayo yamemuweka nje ya uwanja na kumfanya akose michezo kadhaa ikiwa ni pamoja na mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahly.

Mwinyi amesema Joshua ni mchezaji mwenye uzoefu mkubwa wa michuano ya kimataifa na amekuwa akicheza kabla hata yeye (Mwinyi) hajaanza kucheza na alikuwa kwenye kiwango bora kwenye mchezo wa marudiano ugenini dhidi ya Alhly.

Abubar Kisandu amezungumza na mlinzi huyo wa kushoto wa Yanga na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ambaye bado anaendea kuuguza majera yake visiwani Zanzibar akiwa amepewa mapumziko ya muda.

“Kwanza mchezo ulikuwa mgumu kwasababu nyumbani tuli-draw kwahiyo ugenini mchezo ulikuwa ni wa ushindani lakini timu yetu ilicheza vizuri”, anasema Haji Mwinyi ambaye tangu atue Yanga amekuwa tishio kwa nafasi ya Oscar Joshua ambaye mara nyingi amekuwa akianzia benchi.

“Sioni kama kuna pengo, Oscar Joshua alicheza vizuri kwasababu yeye ni mzoefu kuliko hata mimi, yeye alianza kucheza kabla yangu  na kwenye mchezo dhidi ya Al Ahly alicheza vizuri sana”.

Comments