Skip to main content

Marcus Rashford aonesha kuwa na mazungumzo na Roc Nation Sports ya Jay Z

Jay Z anataka kumsajili Marcus Rashford




Imeripotiwa Jay Z anataka kumsajili Marcus Rashford kwenye kampuni yake ya usimamizi wa michezo baada ya kung’ara Manchester United msimu huu
Kampuni ya rapa huyo wa Marekani Roc Nation Sports inasemekana imeanza kujenga uhusiano wa karibu na nyota huyo mwenye miaka 18.
Rashford ana magoli manne katika mechi saba za ligi alizocheza tangu alipoingia kwenye kikosi cha kwanza Man United  mwisho wa mwezi Februari na aliwashusha daraja Aston Villa katika mechi iliyopigwa Jumamosi Old Trafford.
Kwa mujibu wa The Sun, Roc Nation imefanya mazungumzo ya awali na familia ya Rashford kuhusu kumuingiza kwenye rosta ambayo yumo pia beki wa Bayern Munich Jerome Boateng na mwana masumbwi wa Marekani Andre Ward.
Rashford anatarajiwa kusaini mkataba mpya United majira ya joto ambao utaupandisha ujira wake hati paundi 15,000 kwa wiki.

Comments