Skip to main content

MALI ZILIZOMZIMISHA GWAJIMA!

Gari lake la kifahari.
Nyumba yake ya kifahari.
 Helkopta yake.
 
 Magari ya kubebea waumini.
Magari ya wachungaji.
KWA wiki moja sasa, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti kwamba, kujisikia kizunguzungu hatimaye kuanguka na kupoteza fahamu kulikomtokea Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima wakati akihojiwa na polisi kulitokana na kuulizwa maswali yaliyohusu namna alivyozipata mali zake, Risasi Jumamosi linakupa zaidi.
Machi 28, mwaka huu Mchungaji Gwajima alipojisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maaalum ya Dar es Salaam kwa madai ya kumtolea maneno yenye kuudhi Askofu wa Kanisa la Romani Katoliki Jimbo Kuu la Dar, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, alijikuta akizidiwa ghafla na kukimbizwa Hospitali ya TMJ kwa matibabu huku akiwa amepoteza fahamu.
Ilidaiwa kuwa, Gwajima alipokwenda kituoni hapo kujisalimisha alitarajia kukutana na mahojiano ya kuhusu kauli yake ya kumkashifu Kadinali Pengo, lakini matokeo yake akakumbana na maswali ya kuhusu mali zake.
WALIVYOSEMA WATU
"Unajua Gwajima yeye alipoambiwa ajisalimishe Central kwa kumkashifu Pengo alijua akifika pale ataulizwa kwa nini ulimtusi Pengo? Alikukosea nini? Huoni kama yule ni mtu mzima kuliko wewe? Je, uko tayari kumwomba radhi? Lakini matokeo yake katikati ya maswali akaulizwa mali alizonazo alizipata kwa njia gani?"
KWA NINI ALIZIMIA SASA?
"Sasa suala siyo kwamba swali hilo la kuhusu mali lilikuwa na shida kwake, bali lilikuwa la ghafla ndiyo maana akajikuta akichanganyikiwa na kupoteza fahamu," kilisema chanzo kimoja."Wengi wanasema alipoulizwa kuhusu mali alizimia kwa sababu mali zenyewe si halali, hapana! Zile mali ni halali kabisa ila swali halikuwa kwenye mawazo ya Gwajima," kiliendelea kusema chanzo.
RISASI JUMAMOSI LAZICHIMBA
Kufuatia madai hayo, Risasi Jumamosi liliamua kuzama kazini na kuzichimba mali hizo kwa nia ya kuzitambua ambapo uchunguzi wa kina uliofanywa ulibaini kwamba, Mchungaji Gwajima anamiliki gari la kifahari aina ya Hummer 2 ambalo gharama ya manunuzi mpaka kufika Tanzania ni wastani wa shilingi milioni 250.
Mbali na gari hilo la kifahari, Gwajima amewanunulia wachungaji wake 30 magari ya kutembelea ili kupambana na tatizo la usafiri jijini Dar
MAGARI YAANIKWA
Baadhi ya magari hayo ni Subaru Forester (sokoni linauzwa shilingi milioni 17), Mitsubishi Pajero (shilingi milioni 16), Toyota Spacio new model (milioni 20) na Toyota Harrier Lexus (milioni 35).
MJENGO WA MAANA
Risasi Jumamosi lilibaini pia kuwa, mchungaji huyo anaishi kwenye nyumba yake ya kifahari ya ghorofa nne iliyopo Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.
MABASI 20
Kweli Gwajima ni tajiri kwani Risasi Jumamosi likabaini kuwa, pia anamiliki mabasi 20 ambayo ni kwa ajili ya kuwabeba waumini wa kanisa lake wakati wa kwenda kwenye ibada na kurudi makwao katika sehemu mbalimbali za Jiji la Dar. Mabasi hayo kila moja alilinunua kwa shilingi milioni mia moja na ishirini.
PIA KUNA HELKOPTA
Pia, miezi ya hivi karibuni, Gwajima alinunua helkopta (chopa) kwa ajili ya kuzungukia sehemu mbalimbali nchini kutoa huduma ya kiroho. Uzinduzi wa helkopta hiyo ulifanywa na mbunge wa Monduli (CCM) na waziri mkuu wa zamani, mheshimiwa Edward Lowassa.
ANAONGOZA KWA KUWA NA WAUMINI WENGI
Uchunguzi pia ulibaini kwamba, Kanisa la Mchungaji Gwajima linaongoza kwa kuwa na waumini wengi ambapo wanakadiriwa kufikia 70, 000. Kwa maana hiyo sasa, kama waumini wake watatoa sadaka ya Jumapili kila mmoja kwa shilingi elfu mbili, atakuwa anaingiza shilingi milioni 140 kwa ibada moja.Kwa mwezi, Gwajima atakuwa anaingiza shilingi milioni 560 japokuwa wapo waumini inadaiwa hutoa hadi shilingi laki tano (500,000) kama sadaka kwa ibada moja.
MSAMAHA WA KODI
KWA mujibu wa sheria za nchi, baadhi ya taasisi zimepewa msamaha wa kodi wakati wa kuingiza bidhaa mbalimbali nchini, hasa zinazohusu huduma kwa jamii. Bidhaa hizo ni pamoja na magari (Tax Exemption). Taasisi hizo ni pamoja na za dini, elimu, afya (madaktari) na nyingine zenye kuhudumia jamii.
 "Kwa hiyo Gwajima anaweza kumiliki mali nyingi kwa sababu anao msamaha wa kodi, anaweza kuingiza magari mengi kwa kodi ndogo sana," alisema mmoja wa waumini wa Kanisa la Gwajima.
MKEWE ANASEMAJE?
Kwa mujibu wa mke wa Gwajima, Grace alipozungumza na vyombo vya habari hivi karibuni, alisema suala la mumewe kuzimia waulizwe polisi."Mume wangu aliondoka mzima kabisa, polisi ndiyo waulizwe kwa nini alizimia." CHANZO: GLP (Muro)

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.