Skip to main content

Escrow yampa tuzo Kafulila


Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, ametunukiwa tuzo ya kutambua harakati zake za kutetea haki za binadamu katika mazingira hatarishi nchini, likiwamo sakata la uchotwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Alikabidhiwa tuzo hiyo jana ikiwa imepita takriban mwaka mmoja tangu aibue bungeni kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ya uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 200 kifisadi kwenye akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Kashfa ya akaunti hiyo ilihusisha baadhi ya maofisa waandamizi wa serikali, wakiwamo mawaziri, katibu mkuu wa wizara, aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG), viongozi wa dini na majaji.
Mbali na Kafulila, wengine waliotunukiwa tuzo kama hiyo, ni pamoja na waliokuwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba (BMK); Salma Said na Adil Mohamed.
‘Wajumbe’ hao walitunukiwa tuzo hiyo kutokana na kuwa kati ya watu waliokuwa wakifuatiliwa na mtu asiyefahamika kutokana na kutuhumiwa kuipigia kura ya hapana katiba inayopendekezwa katika Bunge hilo.
Mwingine aliyetunukiwa tuzo kama hiyo ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Wafugaji Wanawake Loliondo, Maanda Ngoitick, ambaye alifikia kudhalilishwa kwa kuitwa kuwa siyo raia wakati akiwatetea wanawake wa jamii hiyo.
Tuzo hizo zilizo andaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) zilitolewa katika maadhimisho ya Siku ya Watetezi wa Haki za Binadamu Duniani, jijini Dar es Salaam jana.
Harakati zao hizo zimetambuliwa na Ripoti ya Hali ya Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania ya Mwaka 2014 iliyotolewa na THRDC jana.
Katika maadhimisho hayo, maonyesho ya mashirika, taasisi, wadau, watetezi, wanaharakati, kikiwamo Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Jukwaa la Katiba (Jukata) na Jumuiya ya Ulaya (EU) na Chama cha Albino Tanzania (TAS), yalizinduliwa.
Mgeni rasmi katika maadhimisho alikuwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Tom Bahame Bahame, ambaye alisema tume yake imejipanga kuzishirikisha taasisi mbalimbali katika kuhakikisha maadili ya uongozi yanafuatwa.
Alisema pia itahakikisha haki ya kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na ushiriki wa wananchi katika mchakato wa upigaji kura katika uchaguzi mkuu, mwaka huu.
Chanzo: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...