Skip to main content

Escrow yampa tuzo Kafulila


Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, ametunukiwa tuzo ya kutambua harakati zake za kutetea haki za binadamu katika mazingira hatarishi nchini, likiwamo sakata la uchotwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Alikabidhiwa tuzo hiyo jana ikiwa imepita takriban mwaka mmoja tangu aibue bungeni kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ya uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 200 kifisadi kwenye akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Kashfa ya akaunti hiyo ilihusisha baadhi ya maofisa waandamizi wa serikali, wakiwamo mawaziri, katibu mkuu wa wizara, aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG), viongozi wa dini na majaji.
Mbali na Kafulila, wengine waliotunukiwa tuzo kama hiyo, ni pamoja na waliokuwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba (BMK); Salma Said na Adil Mohamed.
‘Wajumbe’ hao walitunukiwa tuzo hiyo kutokana na kuwa kati ya watu waliokuwa wakifuatiliwa na mtu asiyefahamika kutokana na kutuhumiwa kuipigia kura ya hapana katiba inayopendekezwa katika Bunge hilo.
Mwingine aliyetunukiwa tuzo kama hiyo ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Wafugaji Wanawake Loliondo, Maanda Ngoitick, ambaye alifikia kudhalilishwa kwa kuitwa kuwa siyo raia wakati akiwatetea wanawake wa jamii hiyo.
Tuzo hizo zilizo andaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) zilitolewa katika maadhimisho ya Siku ya Watetezi wa Haki za Binadamu Duniani, jijini Dar es Salaam jana.
Harakati zao hizo zimetambuliwa na Ripoti ya Hali ya Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania ya Mwaka 2014 iliyotolewa na THRDC jana.
Katika maadhimisho hayo, maonyesho ya mashirika, taasisi, wadau, watetezi, wanaharakati, kikiwamo Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Jukwaa la Katiba (Jukata) na Jumuiya ya Ulaya (EU) na Chama cha Albino Tanzania (TAS), yalizinduliwa.
Mgeni rasmi katika maadhimisho alikuwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Tom Bahame Bahame, ambaye alisema tume yake imejipanga kuzishirikisha taasisi mbalimbali katika kuhakikisha maadili ya uongozi yanafuatwa.
Alisema pia itahakikisha haki ya kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na ushiriki wa wananchi katika mchakato wa upigaji kura katika uchaguzi mkuu, mwaka huu.
Chanzo: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.