Skip to main content

Wabunge Saed Kubenea na Anthony Komu wamevuliwa nafasi zao za uongozi Chadema


Wabunge wa chama kikuu cha Upinzani Tanzania Chadema, Saed Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini) leo Alhamisi Oktoba 18, 2018 wamevuliwa nafasi zao za uongozi.


Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika ametangaza uamuzi huo leo katika mkutano na waandishi wa habari ambao wabunge hao waliutumia kuomba radhi juu ya mpango wao hasi dhidi ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob wakibainisha hawakuwa na nia Mnyika alikuwa akisoma maazimio ya kikao cha kamati kuu kilichowahoji wabunge hao jana Jumatano Oktoba 17, 2018.
Tokeo la picha la mnyika
Amesema wabunge hao pia wamevulia uongozi ndani ya chama hicho huku wakiwekwa kwenye kipindi cha uangalizi wa miezi 12.

Kubenea na Komu katika siku za hivi karibuni wamezua mjadala ndani na nje ya chama hicho kwa kile kinachodaiwa kuwa ni sauti yao iliyokuwa ikisikika wakipanga mpango hasi dhidi ya Jacob.

Wabunge hao kwa nyakati tofauti wamekana kuhusika na sauti hizo kwa kile walichoeleza ni za kutengeneza huku Jacob ambaye ni Diwani wa Ubungo (Chadema) naye akieleza kupeleka suala hilo ndani ya chama.
Lakini leo wamekiri kuwa sauti hizo ni zao na kuomba radhi wakibainisha kuwa hawakuwa na nia ovu.

Akisoma maazimio ya kamati kuu Mnyika amesema, “kamati kuu iliitishwa na ikafanya kikao chake juu ya tuhuma za utovu wa nidhamu wa wabunge hawa.”

“Baada ya kuhojiwa hatimaye kamati kuu ilifikia uamuzi na kuwakuta na hatia ya ukiukwaji wa kanuni na maadili ya chama. Imewapa onyo kali kuwataka waandike barua ya kuomba radhi kwa chama na kwa watajwa kufuatia maneno yaliyozungumzwa.”

Akizungumza baada ya Mnyika kumaliza kusoma maazimio hayo, Kubenea amesema, “kama ambavyo mmelezwa nichukue nafasi hii kusema kwamba yaliyotokea siku hiyo ni bahati mbaya na hatukuwa na nia yoyote ovu kwa msingi huo naomba radhi wote walioguswa na watanzania kwa jumla.”

Kwa upande wake Komu amesema, “nichukue nafasi hii kwanza kwa kukishukuru chama kwa jinsi ilivyolichukulia jambo hili na kulipa uzito.”

“Chama ni kikubwa kuliko sisi wote na sisi ni vyombo vya chama, chama kina mikono yake. Kwa kutambua sisi ni vyombo vya chama tunatekeleza maagizo na tayari tumeshaandika barua za kuomba radhi.”

Komu amesema, “tunaomba radhi watanzania yale mazungumzo yetu yalikuwa ya faragha ila teknolojia ikatuzidi yakasambaa unajua mnavyokuwa kwenye faragha mnajiachia. Kwa hayo yaliyotokea tunaomba radhi, tunataka kuanza ukurasa mpya bila kuwa na kigugumizi.”

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...