Skip to main content

Wabunge Saed Kubenea na Anthony Komu wamevuliwa nafasi zao za uongozi Chadema


Wabunge wa chama kikuu cha Upinzani Tanzania Chadema, Saed Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini) leo Alhamisi Oktoba 18, 2018 wamevuliwa nafasi zao za uongozi.


Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika ametangaza uamuzi huo leo katika mkutano na waandishi wa habari ambao wabunge hao waliutumia kuomba radhi juu ya mpango wao hasi dhidi ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob wakibainisha hawakuwa na nia Mnyika alikuwa akisoma maazimio ya kikao cha kamati kuu kilichowahoji wabunge hao jana Jumatano Oktoba 17, 2018.
Tokeo la picha la mnyika
Amesema wabunge hao pia wamevulia uongozi ndani ya chama hicho huku wakiwekwa kwenye kipindi cha uangalizi wa miezi 12.

Kubenea na Komu katika siku za hivi karibuni wamezua mjadala ndani na nje ya chama hicho kwa kile kinachodaiwa kuwa ni sauti yao iliyokuwa ikisikika wakipanga mpango hasi dhidi ya Jacob.

Wabunge hao kwa nyakati tofauti wamekana kuhusika na sauti hizo kwa kile walichoeleza ni za kutengeneza huku Jacob ambaye ni Diwani wa Ubungo (Chadema) naye akieleza kupeleka suala hilo ndani ya chama.
Lakini leo wamekiri kuwa sauti hizo ni zao na kuomba radhi wakibainisha kuwa hawakuwa na nia ovu.

Akisoma maazimio ya kamati kuu Mnyika amesema, “kamati kuu iliitishwa na ikafanya kikao chake juu ya tuhuma za utovu wa nidhamu wa wabunge hawa.”

“Baada ya kuhojiwa hatimaye kamati kuu ilifikia uamuzi na kuwakuta na hatia ya ukiukwaji wa kanuni na maadili ya chama. Imewapa onyo kali kuwataka waandike barua ya kuomba radhi kwa chama na kwa watajwa kufuatia maneno yaliyozungumzwa.”

Akizungumza baada ya Mnyika kumaliza kusoma maazimio hayo, Kubenea amesema, “kama ambavyo mmelezwa nichukue nafasi hii kusema kwamba yaliyotokea siku hiyo ni bahati mbaya na hatukuwa na nia yoyote ovu kwa msingi huo naomba radhi wote walioguswa na watanzania kwa jumla.”

Kwa upande wake Komu amesema, “nichukue nafasi hii kwanza kwa kukishukuru chama kwa jinsi ilivyolichukulia jambo hili na kulipa uzito.”

“Chama ni kikubwa kuliko sisi wote na sisi ni vyombo vya chama, chama kina mikono yake. Kwa kutambua sisi ni vyombo vya chama tunatekeleza maagizo na tayari tumeshaandika barua za kuomba radhi.”

Komu amesema, “tunaomba radhi watanzania yale mazungumzo yetu yalikuwa ya faragha ila teknolojia ikatuzidi yakasambaa unajua mnavyokuwa kwenye faragha mnajiachia. Kwa hayo yaliyotokea tunaomba radhi, tunataka kuanza ukurasa mpya bila kuwa na kigugumizi.”

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.