Skip to main content

Uturuki kutoa ushahidi wa kanda ya sauti inayodai kuwa mwanahabari wa Saudi Arabia aliuawa

Marekani imeomba Uturuki kutoa ushahidi wa kanda ya sauti inayodai kuwa mwanahabari wa Saudi Arabia Jamal Khashoggi aliuawa ndani ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini Istanbul. Rais Trump amewaambia waandishi katika ikulu ya White House kuwa, “Tumeomba kupewa nakala kanda hiyo, kama ni kweli ipo,”.


Bwana Khashoggi hajawahi kuonekana tangu alipoingia jengo la ubalozi wa Saudi Arabia tarehe mbili mwezi huu wa Oktoba.  Saudi Arabia amekanusha madai yakuhusika na kutoweka kwa mwandishi huyo.
Huku hayo yakijiri, Gazeti la Washington Post limechapisha makala ya mwisho yaliyoandikwa na bwana Khashoggi kabla ya kutoweka kwake. Katika makala hayo anazungumzia umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari katika eneo la Mashariki ya kati.
Mhariri wa kimataifa wa gazeti hilo Karen Attiah amesema uchapishaji wa makala hayo ulisitishwa kwa ajili ya kuwa na matumaini kwamba bwana Khashoggi atarejea salama. Aliandika akisema “Sasa sina budi kukubali: Kwamba hilo halitafanyika. Hii ndio makala yake ya mwisho nitakayosahihisha”.

Bi Attiah pia aliongezea kusema, “Makala haya yanaangazia kwa kina kujitolea kwake kupigania uhuru katika mataifa. Uhuru ambao alipigania kwa maisha yake.”
Kuwepo kwa ushahidi kwamba bwana Khashoggi – mkosoaji mkuu wa viongozi wa Saudi – aliuawa kulifichuliwa na wachunguzi wa Uturuki. Ripoti katika vyombo vya habari vya taifa hilo zinaelezea taarifa za kutisha za dakika za mwisho za mwandishi huyo. Gazeti moja la Uturuki linasema sauti ya balozi wa Saudi Arabia mwenyewe Mohammed al Otaibi inasikika katika kanda hiyo iliyonasa kifo cha bwana Khashoggi.
Yeni Safak, ambayo ina uhusianaop wa karibu na serikali imemnukuu balozi huyo akidai kuwa Saudia ilituma maajenti mjini Istanbul: “Msiseme hili. Mtanitia mashakani.”

Bwana Otaibi alirejea mjini Riyadh siku ya Jumanne.
Saudi Arabia ni moja ya washirika wa karibu wa Washington na kupotea kwa Khashoggi kumeiweka utawala huo katika hali ya kutatanisha. Akigusia sauti iliyorekodiwa na ambayo inadaiwa kuwa na ushahidi wa mauaji ya Khashoggi ,Trump aliongeza: “Sina uhakika ya kuwepo kwa sauti hiyo, lakini huenda ikawa ni kweli ipo.”
Bwana Trump amesema anatarajia ripoti kutoka kwa waziri wa wake wa mambo ya nje Mike Pompeo ambaye alikua nchini Saudi Arabia na Uturuki. Rais Trump amesema ukweli kuhusiana na suala hilo utajulikana “Kufikia mwisho wa wiki”.  Amekanusha madai kwamba anajaribu kusaidia Saudi Arabia kutakasa jina lake: “Hapana, hilo haliwezekani, Kile ninachofanya ni kufahamu kile kinachoendelea.”
Katika kipindi cha siku chache zilizopita Trump amegusia uwezekano wa “Wauaji katili” kuhusika na kutoweka kwa mwandishi Jamal Khashoggi. Pia aliwaomba watu kutokimbia kuwalaumu viongozi wa Saudia kabla ya kuthibitisha kuhusika kwa viongozi hao katika kisa hiki.


Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, siku ya Jumatano na Alhamisi, kundi la maafisa wa wachungizi wa Uturuki walipekua makaazi ya balozi wa Saudi Arabia mjini Istanbul kwa karibu saa tisa na baadae kuelekea katika jengo la ubalozi lililopo mita 200 kutoka makaazi hayo.
Kundi hilo la wachunguzi lilihusisha viongozi wa mashtaka pamoja na watalamu wa upasuaji waliokuwa wamevalia mavazi meupe. Magari kadhaa ya Saudia yaliyo na nambari ya usajili ya kidiplomasia yalinaswa katika picha ya CCTV yakiingia makaazi ya balozi chini ya saa mbili baada ya bwana Khashoggi kuingia ubalozi huo siku alipotoweka.
Ubalozi huo ulipekuliwa kwa mara ya kwanza siku ya Jumatatu. Siku ya Jumanne waziri wa mambo ya nje wa Marekani alisafiri mjini Riyadh kufanya mazungumzo na mfalme Salman wa Saudi Arabia na mwanamfalme Mohammed bin Salman, ambaye amekanusha vikali kuhusika kwake na kotoweka kwa mwanahabari Jamal Khashoggi.
Chanzo BBC

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...