Skip to main content

Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini fanya ziara ya kushtukiza kwenye Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (Udart)

Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini , Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Fortunatus Musilimu amefanya ziara ya kushtukiza kwenye barabara ya Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (Udart) pamoja na Kituo cha Kimara Mwisho cha mabasi hayo na kujionea baadhi ya kero zinazowakumba abiria wa kituo hicho.

Kamanda, Musilimu akiwa na msafara wake alianzia ziara hiyo kwa kuanzia katikati ya mji na kuelekea moja kwa moja kwenye kituo hicho, ambapo msafara huo ukiwa eneo la Jangwani ulibaini madereva wa mabasi kuendesha kwa ziadi ya mwendo wa Kilomita 60 wakati sheria inawataka waendeshe chini ya kilomita 50.

Kupitia chombo maalum cha kupima mwendo walibaini moja ya mabasi hayo kukiuka sheria hiyo katika eneo hilo liliopita kwa kasi hiyo.
Msafara huo ukiwa unakaribia eneo la Magomeni ulibaini pia baadhi ya magari ya kawaida kuvunja sheria za usalama barabarani kwa kutumia barabara ya mradi wa mabasi hayo.

Kamanda wa kikosi hicho (SACP), Musilimu akiwa katika Kituo cha Kimara Mwisho ilimchukua muda mrefu kuangalia huduma ya usafiri inavyotolewa na Udart kupitia abiria waliokuwa wakielekea Kivukoni na Gerezani, akiwa kituoni alipata fursa ya kuzungumza na baadhi ya abiria waliomueleza kero zao.

Mmoja wa abiria aliyekuwa akielekea Kivukoni, Poza Hassan alimuelezea kamanda huyo kuwa hali huwa ngumu nyakati za asubuhi ambapo abiria hupata adha kubwa wakati wa kupanda mabasi hayo.

“ Kiukweli kwa mtu wa kawaida ni kero kutumia usafiri huu kwani mrundikano wa abiria ni mkubwa hali inayoonyesha mabasi ni machache wakati wa asubuhi kusababisha watu kukanyagana na kupoteza mali zao,” alisema Poza.

Alisema wakati wa jioni abiria wanaotoka mjini kurudi nyumbani kwao hukumbana na adha ya aina hiyo hiyo ya kugombania mabasi hayo na kuwa pendekezo lake wahusika wafanye utafiti na kupata data ambazo sio za kupika ili kupata majawabu juu ya kero hizo.

Kwa upande wake, abiria Richard Msuya alibainisha kuwepo kero hiyo kila siku huku akisisitiza kuwepo mbadala wa mabasi mengine ya makampuni mengine  ili kuleta ushindani utakaosababisha kuondoa adha hiyo.
“ Mkuu naona hawa jamaa wanafanya hivi sababu hakuna ushindani wapo wenyewe tu kungekuwa na mabasi ya watu wengine yanayoleta ushindani kero zisingekuwepo ni bora warudishe daladala kama zamani ziwaletee changamoto,” alisema Msuya.

Baada ya kusikiliza kero hizo Kamanda na msafara wake aliamua kukagaua baadhi ya mabasi hayo na kubaini makosa mbalimbali ambapo katika basi lenye namba T 109 lilikutwa na kosa kutokuwa na matairi imara likatozwa faini na dereva, William Kasonzo kuagizwa kulirudisha yadi.
Gari jingine lenye namba T 997 DGV liliokuwa linaendeshwa na dereva, Adelaida Nyasi lilibainika kukutwa na faini ya muda mrefu ambayo ilikuwa haijalipwa.

Kamanda, Musilimu baada ya kujionea kero katika ziara aliyoifanya kwa kushtukiza aliagiza uongozi wa Udart kuyashughulikia matatizo hayo yaliyobainishwa na wananchi pamoja na aliyojionea.

“ Nimeshuhudia madereva wanavyoendesha kwa kasi Jangwani hata magari ya abiria kuingia kwenye barabara ya Udart , nachoweza kusema tukimkamata dereva wa namna hiyo tunamfungia leseni yake,” alisema.
Aliongeza kusema kuwa ndani ya mabasi hayo wamebaini kutokuwepo mikanda ya kutosha ya kushikia abiria waliosimama na kukazia watakuwa wakali kwa kutumia staili ya nyakua nyakua.

Naye, Mmoja wa maofisa wa Udart, Joe Beda aliyepewa maelekezo hayo alisema atayafikisha kwa uongozi wa juu ili yatafutiwe ufumbuzi.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...