Skip to main content

Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini fanya ziara ya kushtukiza kwenye Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (Udart)

Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini , Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Fortunatus Musilimu amefanya ziara ya kushtukiza kwenye barabara ya Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (Udart) pamoja na Kituo cha Kimara Mwisho cha mabasi hayo na kujionea baadhi ya kero zinazowakumba abiria wa kituo hicho.

Kamanda, Musilimu akiwa na msafara wake alianzia ziara hiyo kwa kuanzia katikati ya mji na kuelekea moja kwa moja kwenye kituo hicho, ambapo msafara huo ukiwa eneo la Jangwani ulibaini madereva wa mabasi kuendesha kwa ziadi ya mwendo wa Kilomita 60 wakati sheria inawataka waendeshe chini ya kilomita 50.

Kupitia chombo maalum cha kupima mwendo walibaini moja ya mabasi hayo kukiuka sheria hiyo katika eneo hilo liliopita kwa kasi hiyo.
Msafara huo ukiwa unakaribia eneo la Magomeni ulibaini pia baadhi ya magari ya kawaida kuvunja sheria za usalama barabarani kwa kutumia barabara ya mradi wa mabasi hayo.

Kamanda wa kikosi hicho (SACP), Musilimu akiwa katika Kituo cha Kimara Mwisho ilimchukua muda mrefu kuangalia huduma ya usafiri inavyotolewa na Udart kupitia abiria waliokuwa wakielekea Kivukoni na Gerezani, akiwa kituoni alipata fursa ya kuzungumza na baadhi ya abiria waliomueleza kero zao.

Mmoja wa abiria aliyekuwa akielekea Kivukoni, Poza Hassan alimuelezea kamanda huyo kuwa hali huwa ngumu nyakati za asubuhi ambapo abiria hupata adha kubwa wakati wa kupanda mabasi hayo.

“ Kiukweli kwa mtu wa kawaida ni kero kutumia usafiri huu kwani mrundikano wa abiria ni mkubwa hali inayoonyesha mabasi ni machache wakati wa asubuhi kusababisha watu kukanyagana na kupoteza mali zao,” alisema Poza.

Alisema wakati wa jioni abiria wanaotoka mjini kurudi nyumbani kwao hukumbana na adha ya aina hiyo hiyo ya kugombania mabasi hayo na kuwa pendekezo lake wahusika wafanye utafiti na kupata data ambazo sio za kupika ili kupata majawabu juu ya kero hizo.

Kwa upande wake, abiria Richard Msuya alibainisha kuwepo kero hiyo kila siku huku akisisitiza kuwepo mbadala wa mabasi mengine ya makampuni mengine  ili kuleta ushindani utakaosababisha kuondoa adha hiyo.
“ Mkuu naona hawa jamaa wanafanya hivi sababu hakuna ushindani wapo wenyewe tu kungekuwa na mabasi ya watu wengine yanayoleta ushindani kero zisingekuwepo ni bora warudishe daladala kama zamani ziwaletee changamoto,” alisema Msuya.

Baada ya kusikiliza kero hizo Kamanda na msafara wake aliamua kukagaua baadhi ya mabasi hayo na kubaini makosa mbalimbali ambapo katika basi lenye namba T 109 lilikutwa na kosa kutokuwa na matairi imara likatozwa faini na dereva, William Kasonzo kuagizwa kulirudisha yadi.
Gari jingine lenye namba T 997 DGV liliokuwa linaendeshwa na dereva, Adelaida Nyasi lilibainika kukutwa na faini ya muda mrefu ambayo ilikuwa haijalipwa.

Kamanda, Musilimu baada ya kujionea kero katika ziara aliyoifanya kwa kushtukiza aliagiza uongozi wa Udart kuyashughulikia matatizo hayo yaliyobainishwa na wananchi pamoja na aliyojionea.

“ Nimeshuhudia madereva wanavyoendesha kwa kasi Jangwani hata magari ya abiria kuingia kwenye barabara ya Udart , nachoweza kusema tukimkamata dereva wa namna hiyo tunamfungia leseni yake,” alisema.
Aliongeza kusema kuwa ndani ya mabasi hayo wamebaini kutokuwepo mikanda ya kutosha ya kushikia abiria waliosimama na kukazia watakuwa wakali kwa kutumia staili ya nyakua nyakua.

Naye, Mmoja wa maofisa wa Udart, Joe Beda aliyepewa maelekezo hayo alisema atayafikisha kwa uongozi wa juu ili yatafutiwe ufumbuzi.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...