Skip to main content

Rais Kagame afanya mabadiliko baraza lake la mawaziri


Rais Paul Kagame akizungumza na wanahabari wakati wa mkutano wa mataifa yanayozungumza Kifaransa Yerevan mnamo Oktoba 12, 2018
 Rais wa Rwanda Paul Kagame

Rais wa Rwanda Paul Kagame amefanya mabadiliko makubwa katika baraza lake la mawaziri na kumteua Dkt Richard Sezibera kuwa waziri mpya wa mashauri ya nchi za nje.
Jenerali James Kabarebe aliyekuwa mtu wa karibu sana na Rais Kagame amepoteza wadhifa wake kama waziri wa ulinzi na badala yake akateuliwa mshauri wa rais katika masuala ya usalama.

Katika mabadiliko makubwa na ya kushtukiza aliyofanya Rais Kagame wizara 8 kati ya 23 zimepata mawaziri wapya zikiwemo wizara nyeti tatu, wizara ya ulinzi ambayo sasa inaongozwa na Meja jenerali Albert Murasira aliyechukua nafasi ya Jenerali James Kabarebe.
Mwandishi wa BBC Yves Bucyana anasema si wengi walitarajia mabadiliko haya.
Jenerali Kabarebe ambaye amepewa nafasi ya kuwa mshauri maalumu wa rais wa maswala ya ulinzi na jeshi alikuwa mshirika wa karibu sana na Rais Paul Kagame tangu vita vilivyong'oa utawala wa rais Juvenali Habyarimana miaka ya 1990.
 
Image caption Jenerali James Kabarebe alipokuwa mkuu wa majeshi ya Rwanda mwaka 2005
Tangu RPF kushika hatamu akachukua nyadhifa nyeti za utawala wa jeshi.

Comments