Skip to main content

Maadhimisho ya miaka 50 ya ushirikiano baina ya China na Tanzania yaliyofanyika Dar es Salaam


Serikali ya Tanzania imeipongeza serikali ya watu wa china kwa ushirikiano mzuri wenye manufaa katika seka ya afya nchini.
Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Mambo ya nje ,kikanda na ushirikiano wa afrika mashariki wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya ushirikiano baina ya China na Tanzania yaliyofanyika Dar es Salaam.


Dk.Mahiga aliwaeleza washiriki katika hafla hiyo kuwa  China ilionesha nia thabiti kuisadia Tanzania katika mambo mbalimbali baada yakupata Uhuru kutoka kwa wakoloni na mwaka 1968 nchi hizo mbili zilisaini hati ya makubaliano ya kushirikiana katika sekta ya afya.
 Amesema kuwa pamoja nakupokea misaada mbalimbali kutoka China ,Tanzania nayo ina mchango na msaada mkubwa kwa Taifa hilo linalo kadiriwa kuwa Taifa la pili kwa uchumi unaokuwa kwa haraka baada ya Marekani.
“China imefanya mengi kwetu lakini katika sekta ya afya imetusaidia sana kwakuwapa madaktari wetu mafunzo huko china tokea kuanzishwa kwa mashirikiano haya ,hata sisi pia tunaisaidia China kwa mambo mengi,1974 wakati kura ya VETO ya Umoja wa Mataifa Mwalimu Nyerere alihamasisha wa afrika kupigia kura China kuwa mjumbe kudumu wa baraza la usalama la UN,”amesema
Naye Balozi wa China Tanzania Wang Ke alisema kuwa hadi sasa China imeleta madaktari 53 ambapo 11 walikula kiapo jana cha kuhudumu katika hospitali mbalimbali nchini ikiwemo Muhimbi,hospital ya rufaa ya Mbeya na Taasis ya Moyo ya Jakaya Kikwete watakao hudumu zaidi katika magonjwa yasiyo yakuambukizwa.
kuanzishwa kwa mashirikiano hayo madaktari 1,470 wamehuduma Tanzania pamoja na changamoto mbalimbali hadi sasa jumla ya wagonjwa 300,000 wametibiwa na madaktari hao ,Balozi huyo amesema kuwa China itaendelea kushirikiana na Tanzania kutoa huduma.
“Malengo yetu ni kuokoa maisha ya ndugu zetu watanzania na tumeanza kuwafikia watu wa vijijini zaidi ambapo madaktari wetu wanatoa huduma katika mikoa mbalimbali kama Mtwara, Mara, Kigoma na Mbeya na tunaendelea kupanua huduma ya afya iwafikie wananchi wengi kadri iwezekanavyo,”amesema
Kwa upande wake Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii    Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu alisema kuwa watahakikisha ushirikiano huo unaendelea baina ya nchi hizo mbili kwakuwa una manufaa kwa maisha ya watanzania.
“Tutaendelea kushirikiana na ndugu zetu wa china katika sekta ya afya ili tuokoe maisha watanzania wengi kwakutoa huduma za kitabibu hapa nchi nakuepuka kuwasafirisha wagonjwa wetu nje nchi kwa ajili ya matibu,”amesema
Waziri Ummy ameongeza  kuwa dhamira kubwa ya serikali kwa sasa nikuboresha mazingira ya afya nchini kwa kusomesha madaktari wengi lakini aliongeza kuwa wahandisi wa vifaa vya afya nao ni muhimu sana.
Alisema kuanzishwa kwa mashirikiano hayo China imeshirikiana katika mambo mbalimbali kiuchumi,kisiasa na kijamii, ambapo china imekuwa mstari wa mbele sana katika matukio mbalimbali ya kijamii yakiwemo mafuriko na maafa mbalimbali.

Comments