Skip to main content

Rwanda yaondoa watoto jeshini lakini inawaandikisha kwa M23



rwanda ed3f8
Katika kipindi cha miaka 16 iliyopita nchi ya Rwanda imefanikiwa kuondoa kutoka jeshini wanajeshi watoto wapatao 3,000. Lakini wakati juhudi hizi zinaendelea Umoja wa Mataifa unasema Kigali imekuwa ikilisaidia kundi moja la waasi kutoka Congo la M23 kuwaandikisha watoto nchini Rwanda na kuwapeleka kuungana na waasi wa M23 kushiriki katika mapambano Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. (HM)

Comments