Katika kipindi cha miaka 16 iliyopita
nchi ya Rwanda imefanikiwa kuondoa kutoka jeshini wanajeshi watoto
wapatao 3,000. Lakini wakati juhudi hizi zinaendelea Umoja wa Mataifa
unasema Kigali imekuwa ikilisaidia kundi moja la waasi kutoka Congo la
M23 kuwaandikisha watoto nchini Rwanda na kuwapeleka kuungana na waasi
wa M23 kushiriki katika mapambano Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. (HM)
Comments