Skip to main content

Mwigulu awasihi waTanzania wa Uingereza kutumia upeo waliyonayo kulisaidia taifa zaidi kimaendeleo kuliko kuwa na ushabiki wa siasa


Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa na Mbunge wa Iramba Magharibi Mh. Mwigulu Lameck Nchemba akisisitiza Jambo katika hotuba yake aliyoitoa hapa nchini Uingereza iliyojaa mapenzi na Tanzania zaidi ya Itikadi na kupokelewa vyema na watanzania wengi hapa UK.
Mabadiliko hayatakuja kwa kubadilisha vyama bali ni nia zenu {Mindset) zikifanywa kuwa mpya na mapenzi ya nchi yenu.”
Katika hali iliyotajwa kuwa ni ya furaha, kutokana na changamoto zilizokuwepo siku ya jumamosi jijini Leicester Uingereza, kijana shupavu na “JEMBE” la kujivunia katika Taifa la Tanzania Naibu Katibu Mkuu wa CCM Taifa, na Mbunge wa Ilamba Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba akiambatana na mshauri wa Rais mheshimiwa Rajabu Luhwavi, kwa pamoja waliweza kutoa majibu ya changamoto nyingi zinazolikabili Taifa kwa watanzania wengi waliojitokeza katika mkutano mkubwa uliohudhuriwa na watanzania wengi kutoka maeneo mbali mbali ya Uingereza.
Ujasiri, uwazi na ukweli wa mambo ya kiutendaji katika taifa letu ndio hasa imekuwa ni chachu na kivutio kikubwa kwa watanzania wengi waliohudhuria mkutano huo mkubwa jiji Leicester ambapo Mh. Mwigulu Nchemba aliweza kuweka wazi mengi ambayo serikali imeweza kuyafanya katika upande wa Elimu, Miundo mbinu na huduma za afya kwa watanzania pia kutoa kasoro katika maeneo yanayokuwa vikwazo katika kutoa huduma bora.
“Nchi yetu ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya, mojawapo ya mambo ambayo tunayafanyia kazi ni suala la uraia pacha. Ni pendekezo lililowakirishwa na Chama Cha Mapinduzi katika baraza zake za uchangiaji maoni ya Katiba mpya. CCM inawajali watanzania wote hivyo ikaona ni vyema na nyinyi mlioko ughaibuni kupata fursa sawa za kimaendeleo katika nchi yenu” alisema Mhe. Mwigulu Nchemba.
Untitled 8
Mheshimiwa Nchemba aliendelea na kusema kwamba nchi yetu inapita katika kipindi cha mabadiliko. Idadi ya watanzania imeongezeka kwa kiasi kikubwa na wengi wa ongezeko hili ni vijana ambao ni watafutaji na wajasiliamali wengi. Kuna haja kubwa kama chama kubuni taratibu nzuri za kimaendeleo ili kuendana na wimbi hili la ongezeko la watu.
Mheshimiwa Nchemba kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi aliwasihi watanzania waishio Uingereza kutumia upeo (Exposure) waliyonayo katika kulisaidia taifa kupiga hatua zaidi za kimaendeleo kuliko kuwa na ushabiki wa siasa kama ilivyo kwa baadhi ya wanasiasa nyumbani na badala yake wawe chemichemi ya mawazo ya kimaendeleo katika nchi yao.


Comments