Skip to main content

Ripoti ya upelelezi ya Kenya yaonyesha usumbuaji wa uwepo wa al-Shabaab huko Garissa


Ukweli kuhusu kiasi cha uwepo wa al-Shabaab na ushawishi katika kaunti ya Garissa kaskazini mashariki mwa Kenya, ambayo ilionyeshwa katika ripoti iliyovuja ya Shirika la Upelelezi la Taifa (NIS), imewaacha viongozi na wakaazi wa kaunti katika matatizo.

Mwanamke aliyekaa kando ya mtoto aliyejeruhiwa kwenye Hospitali Kuu ya Jimbo la Garissa tarehe 4 Novemba, 2012 baada ya shambulio la guruneti katika kanisa ambalo lilisababisha kifo cha askari polisi mmoja na watu wengine 14 kujeruhiwa. [Stringer/AFP]

"Idadi kubwa ya mashambulio ya kigaidi ambayo Garissa imekumbana nayo ikilinganishwa na kaunti nyingine katika nchi ni uthibitisho kwamba al-Shabaab ni miongoni mwao," Seneta wa Garissa Yusuf Haji aliiambia Sabahi.

"Wakati wa hatua za awali na kwenye kilele cha shambulio, Garissa ilichukuliwa kama makao makuu ya kikundi hiki," alisema, akiongezea kwamba al-Shabaab walihamisha operesheni zao kwenda Kenya baada ya Somalia na vikosi shirika kudhibiti kikundi hicho cha wanamgambo katika ardhi yao ya nyumbani nchini Somalia.

Ripoti ya hali katika kurasa 32 zilizo ndani ya waraka wa NIS, ambayo iliandikwa tarehe 26 Aprili, 2013 lakini ilivuja kwa wananchi baada ya shambulio la al-Shabaab kwenye kituo cha biashara cha Westgate mwezi uliopita, inaelezea ukweli unaosumbua.

Wafanyakazi wa Amniyat, sehemu ya kitengo cha upelelezi cha wasomi cha al-Shabaab, kimechagua Garissa kama "ngome inayopendelewa kwa ajili ya operesheni zao ambapo waliweka miundombinu kuwezesha shughuli zao", kwa mujibu wa ripoti.

Comments