Ukweli kuhusu kiasi cha uwepo wa al-Shabaab na ushawishi katika kaunti
ya Garissa kaskazini mashariki mwa Kenya, ambayo ilionyeshwa katika
ripoti iliyovuja ya Shirika la Upelelezi la Taifa (NIS), imewaacha
viongozi na wakaazi wa kaunti katika matatizo.

Mwanamke aliyekaa kando ya mtoto
aliyejeruhiwa kwenye Hospitali Kuu ya Jimbo la Garissa tarehe 4
Novemba, 2012 baada ya shambulio la guruneti katika kanisa ambalo
lilisababisha kifo cha askari polisi mmoja na watu wengine 14
kujeruhiwa. [Stringer/AFP]
"Idadi kubwa ya mashambulio ya kigaidi ambayo Garissa imekumbana nayo
ikilinganishwa na kaunti nyingine katika nchi ni uthibitisho kwamba
al-Shabaab ni miongoni mwao," Seneta wa Garissa Yusuf Haji aliiambia
Sabahi.
"Wakati wa hatua za awali na kwenye kilele cha shambulio, Garissa
ilichukuliwa kama makao makuu ya kikundi hiki," alisema, akiongezea
kwamba al-Shabaab walihamisha operesheni zao kwenda Kenya baada ya
Somalia na vikosi shirika kudhibiti kikundi hicho cha wanamgambo katika
ardhi yao ya nyumbani nchini Somalia.
Ripoti ya hali katika kurasa 32 zilizo ndani ya waraka wa NIS, ambayo
iliandikwa tarehe 26 Aprili, 2013 lakini ilivuja kwa wananchi baada ya
shambulio la al-Shabaab kwenye kituo cha biashara cha Westgate mwezi
uliopita, inaelezea ukweli unaosumbua.
Wafanyakazi wa Amniyat, sehemu ya kitengo cha upelelezi cha wasomi cha
al-Shabaab, kimechagua Garissa kama "ngome inayopendelewa kwa ajili ya
operesheni zao ambapo waliweka miundombinu kuwezesha shughuli zao", kwa
mujibu wa ripoti.
Comments