Skip to main content

NATAFAKARI UAMUZI WANGU



21.zitoKabwejanaKijijiniMwandiga 3f0e3
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, amesema anatafakari upya uamuzi wake wa kuachana na siasa baada ya kushuhudia hali ngumu ya maisha inayowakabili wananchi wa mkoa wa Tabora.
Alisema kutokana na hali duni ya maisha ya wananchi aliyoishuhudia katika maeneo mbalimbali kwenye majimbo ya Sikonge na Igalula, atahakikisha kwa kushirikiana na viongozi wenzake ndani ya CHADEMA wanakifuta Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Kanda ya Magharibi.
Zitto ambaye alikwishakutangaza kutogombea tena ubunge katika Jimbo lake la Kigoma Kaskazini kwenye Uchaguzi Mkuu ujao, alitoa kauli hiyo juzi katika mikutano ya hadhara, katika majimbo ya Sikonge na Igalula, ukiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya ujenzi wa chama katika kanda hiyo.
Maeneo aliyoyatembelea na kukuta hali ya wananchi ikiwa hairidhishi hususan katika kupata huduma ya maji ni kata za Ipole, Kitunda na Sikonge, zilizo jimboni Sikonge na kata za Miswaki, Kigwa na Loya zilizoko Igalula, wilayani Uyui.
Alisema kuwa licha ya wabunge wa mkoa huo kutokana na chama kinachotawala kwa zaidi ya miaka 50, wamekosa sauti ya kuzungumzia matatizo ya wananchi kwa sababu ya kulinda masilahi binafsi.
Zitto alifafanua kuwa ni jambo la kusikitisha kuona mikoa ya magharibi ikiwa nyuma kimaendeleo licha ya kuchangia kiasi kikubwa cha fedha za kigeni katika pato la taifa kupitia kilimo cha tumbaku.
"Ninatafakari upya uamuzi wangu wa kuachana na siasa, ni vigumu kama sitashirikiana na wenzangu kuhakikisha hali hii ya watu kugombea maji ya kunywa na wanyama katika shimo moja inakwisha," alisema.
Aliwataka wananchi wawaunge mkono pale wanapopambana bungeni hata ikibidi kupanda juu ya meza au kutoka nje pindi masilahi ya watu yanapopuuzwa, kwa sababu ya kuwapo kwa wabunge wengi wa CCM ndani ya Bunge.
Zitto aliongeza kuwa serikali ya CCM imechoka na haiwezi kuongoza na kwamba kama ilishindwa kusimamia reli iliyojengwa na wakoloni haiwezi kuongoza nchi iliyogubikwa na umaskini licha ya kuwa na utajiri kila sehemu.
"Laiti kama mngejua yale tunayoyajua na kuyapigania bungeni hususan ufisadi unaofanywa na serikali ya CCM, naamini wananchi mngeingia barabarani kuhakikisha serikali hii inatoka madarakani," alisisitiza.
Akizungumzia uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kukutana na viongozi wa vyama vya CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi kujadili muswada wa sheria wa Katiba, Zitto alisema ni wazi amedhihirisha kwamba Waziri Stephen Wassira alikuwa akiongea kitu ambacho hakijui.
Alisema wakati wapinzani walipotoka bungeni kupinga muswada huo, Wassira alisimama hadharani na kusema kwamba wapinzani hawatapata fursa nyingine ya kujadiliana na Ikulu kuhusu Katiba.
Akiwa katika Kata ya Loya, Jimbo la Igalula, Zitto alisema kitendo cha serikali kuwanyanyasa wafugaji ni udhalilishaji dhidi ya utu, kwa kuwa kila Mtanzania ana haki ya kuishi sehemu yoyote ili mradi asivunje sheria.
Alisema viongozi wa CCM wamekuwa wakiwatumia wafugaji kama mifuko yao ya hifadhi, kwa kujipatia fedha kinyume cha sheria, hali aliyoelezea kuwa ni ukiukaji wa utawala bora.
Zitto alieleza kusikitishwa na taarifa ya walimu wa Kata ya Loya kuwa wanatumia sh 20,000 kwa ajili ya kuweza kufika barabara kuu ya kuelekea mjini Tabora kufuatilia mishahara yao.CHANZO TANZANIA DAIMA.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.