Skip to main content

MWALIMU NYERERE MWENYE KADI NAMBA MOJA YANGA SC AMBAYE DAIMA ATAKUMBUKWA



nyerere_na_kikwete_na_kalikumtima_0ebe4.jpg
Katikati ni Mwalimu Nyerere akiwa na Katibu wa DABA wa enzi hizo, Jackson Kalikumtima kulia na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Jakaya Kikwete kushoto, sasa rais wa Jamhiri ya Muungano Tanzania. Hii ilikuwa Aprili mwaka 1998 Uwanja wa Ndani wa Taifa, Dar es Salaam.
Na Mahmoud Zubeiry, Bukoba
KADI namba moja ya uanachama wa klabu ya Yanga SC ya Dar es Salaam, inadaiwa alipewa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye leo anatimiza miaka 14 tangu kifo chake, Oktoba 14, mwaka 1999.
Wakati Mwalimu Nyerere anafariki dunia, mimi nilikuwa mwandishi mchanga sana- wakati huo nipo kampuni ya Habari Corporation Limited, chini ya wamiliki wake wa awali akina Jenerali Ulimwengu.
Aliyekuwa bosi wangu wakati huo, Kenny Manara, aliyekuwa Mhariri wa gazeti DIMBA alinipa kazi ya kwenda Uwanja wa Taifa, sasa Uhuru ulipowekwa mwili wa marehemu kwa ajili ya kuagwa ili kuandika habari juu ya wanamichezo waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu na kuchukua maoni yao.

Comments