Skip to main content

Miaka 23 ya kuungana tena kwa Ujerumani



kuungana_kwa_ujerumani_6fac7.jpg
Miaka 23 baada ya kuungana tena kwa Ujeurmani mbili, mabadiliko yanaonekana katika upande wa Ujerumani mashariki. Miundombinu imekuwa bora ikilinganishwa na magharibi, lakini tofauti za kiuchumi bado zingalipo.
Kansela Helmut Kohl, ambaye aliesherekea kuungana tena Ujerumani mbili kwa mara ya kwanza, aliwahi kuwaahidi wakaazi wa majimbo sita ya Ujerumani mashariki mandhari ya kupendeza. Lakini katika miaka ya kwanza ya muungano huo, hali ilikuwa kinyume cha hivyo. Miundombinu chakavu, kufilisika kwa makampuni, viwango vya juu vya ukosefu wa ajira na kuhama kwa vijana kwa wingi, kiasi kwamba baadhi ya maeneo yalitishiwa kubaki matupu. Hivi sasa ni miaka 23 tangu Ujerumani mbili ziungane tena. Je, kuna lililotimia katika ahadi ya Kohl?

Comments