Skip to main content

Jinsi CCM inavyowachukia watetezi wa Umma na kuwabeba wabadhirifu wa mali za Uma


Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imebariki kuondolewa kwa majina ya baadhi ya vigogo wakiwamo wabunge kuwania nafasi ndani ya chama hicho, maamuzi yanayotoa picha ya kung’oa watu wenye tuhuma mbalimbali.
Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya kikao hicho, kazi kubwa ambayo imefanywa na Kamati ya Usalama na Maadili ya chama hicho iliungwa mkono na CC, huku wajumbe wa vikao hivyo viwili wakimpongeza Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuridhia maamuzi magumu.
Kikao cha CC ambacho kilifanyika juzi kuanzia mchana na kumalizika saa 6:30 usiku, kilielekeza shoka lake kwa majina yote ya wabunge waliowania nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ambao walihusika katika utiaji saini azimio la kumung’oa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, mapema mwaka huu.
Wabunge hao walisaini katika fomu maalum iliyoandaliwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, kwa ajili ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu.
Wabunge hao walichukuliwa uamuzi huo ili kuishinikiza serikali kuwafukuza mawaziri ambao wizara zao zilitajwa katika ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Kamati kwa kashfa mbalimbali na kuisababishia serikali hasara.
Wabunge wa CCM waliotia saini ni Nimrod Mkono ambaye ni Mbunge wa Musoma Vijijini, anayewania nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa na; Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe ambaye anagombea ujumbe wa NEC kupitia Wilaya ya Ludewa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina. Wote wamekatwa.
Mwingine ambaye jina lake limekatwa ni Mbunge wa Ilala na Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu ambaye ameomba kupendekezwa kugombea uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa.

Comments