Skip to main content

Nida yatimua wafanyakazi 600, wengine 800 kufuata


Mamlaka ya Vitambulisho imevunja mikataba ya wafanyakazi wake 597 kutokana na ufinyu wa bajeti na ufanisi mdogo katika kuzalisha vitambulisho vya taifa.
Mamlaka hiyo itapitia upya majukumu ya wafanyakazi wengine 802 wa kudumu ili kuendana na majukumu yaliyopo. Kama itabainika idadi bado ni kubwa, watarudishwa wizara ya utumishi kwa ajili ya kupangiwa majukumu mengine.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Nida, Dk Modestus Kipilimba alisema mamlaka hiyo imekuwa na wafanyakazi wengi, lakini kazi iliyokusudiwa ya kutengeneza vitambulisho vya Taifa haifanyiki kikamilifu.
Dk Kipilimbi alisema wafanyakazi 1,399 waliopo Nida walitakiwa kuzalisha vitambulisho 24,000 kwa siku, lakini waliweza kuzalisha vitambulisho 1,200 kwa siku nchi nzima ambayo ni sawa na asilimia tano.
“Kuanzia leo (jana) ninawatangazia watumishi wa mkataba kwamba Nida hakuna kazi kwa sasa. Tutapitia upya masharti ya mikataba yao na kufuata utaratibu wa kisheria,” alisema.
Alisema lengo kubwa la Nida ni kuongeza ufanisi katika utendaji ili kuhakikisha kwamba ifikapo Desemba 31, mwaka huu kila mwananchi awe n kitambulisho chake.
Alisema kuna namna nyingi za utambulisho wa Taifa ikiwa ni pamoja na vitambulisho vyenyewe kuhifadhi taarifa kwenye tanzidata na namba za simu zake.
Mkurugenzi huyo ambaye aliteuliwa Februari 15 kushika wadhifa huo, alisema lengo lao jingine ni kuinua matumizi ya utambulisho wa Taifa.
Katika kutekeleza hilo, alisema watakutana na wadau mbalimbali ili kukifanya kitambulisho cha Taifa kihifadhi taarifa mbalimbali za wananchi.
“Pia, tunafanya uhakiki wa mikataba yote ambayo Nida imeingia ili kujiridhisha kama sheria ya manunuzi ilifuatwa. Kama kuna mikataba ambayo haikufuata taratibu, basi tutaangalia utaratibu wa kisheria,” alisema.
Alisema Nida inatarajia kupokea mashine za BVR 5,000 kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) ili kutumia kutengeneza vitambulisho vya Taifa ambavyo vitakuwa na saini ya mwenye kitambulisho hicho na anayekitoa.
“Tumepokea maoni ya watu wengi wakionyesha umuhimu wa saini kwenye kitambulisho, kama Rais (John) Magufuli alivyosema. Kwa hiyo, tunakamilisha taratibu za kubadilisha kanuni ili vitambulisho tutakavyoendelea kuvitoa viwe na saini,” alisema.
Hata hivyo alisistiza kwamba vitambulisho ambavyo havina saini vitaendelea kutumika na kutambuliwa kwa sababu saini ipo kwenye nyaraka nyingine.
Alisema Nida itaruhusu pia wananchi kwenda kubadilisha na kupata vitambulisho vyenye saini.
Lengo la mabadilikp haya ni kuongeza ufanisi kwa uwajibikaji. Hasara iliyopatikana ni kubwa sana, hatutaki tuendelee kubeba msalaba huu wakati lengo kuu halijatimia,” alisema Dk Kipilimba.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...