Skip to main content

Nida yatimua wafanyakazi 600, wengine 800 kufuata


Mamlaka ya Vitambulisho imevunja mikataba ya wafanyakazi wake 597 kutokana na ufinyu wa bajeti na ufanisi mdogo katika kuzalisha vitambulisho vya taifa.
Mamlaka hiyo itapitia upya majukumu ya wafanyakazi wengine 802 wa kudumu ili kuendana na majukumu yaliyopo. Kama itabainika idadi bado ni kubwa, watarudishwa wizara ya utumishi kwa ajili ya kupangiwa majukumu mengine.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Nida, Dk Modestus Kipilimba alisema mamlaka hiyo imekuwa na wafanyakazi wengi, lakini kazi iliyokusudiwa ya kutengeneza vitambulisho vya Taifa haifanyiki kikamilifu.
Dk Kipilimbi alisema wafanyakazi 1,399 waliopo Nida walitakiwa kuzalisha vitambulisho 24,000 kwa siku, lakini waliweza kuzalisha vitambulisho 1,200 kwa siku nchi nzima ambayo ni sawa na asilimia tano.
“Kuanzia leo (jana) ninawatangazia watumishi wa mkataba kwamba Nida hakuna kazi kwa sasa. Tutapitia upya masharti ya mikataba yao na kufuata utaratibu wa kisheria,” alisema.
Alisema lengo kubwa la Nida ni kuongeza ufanisi katika utendaji ili kuhakikisha kwamba ifikapo Desemba 31, mwaka huu kila mwananchi awe n kitambulisho chake.
Alisema kuna namna nyingi za utambulisho wa Taifa ikiwa ni pamoja na vitambulisho vyenyewe kuhifadhi taarifa kwenye tanzidata na namba za simu zake.
Mkurugenzi huyo ambaye aliteuliwa Februari 15 kushika wadhifa huo, alisema lengo lao jingine ni kuinua matumizi ya utambulisho wa Taifa.
Katika kutekeleza hilo, alisema watakutana na wadau mbalimbali ili kukifanya kitambulisho cha Taifa kihifadhi taarifa mbalimbali za wananchi.
“Pia, tunafanya uhakiki wa mikataba yote ambayo Nida imeingia ili kujiridhisha kama sheria ya manunuzi ilifuatwa. Kama kuna mikataba ambayo haikufuata taratibu, basi tutaangalia utaratibu wa kisheria,” alisema.
Alisema Nida inatarajia kupokea mashine za BVR 5,000 kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) ili kutumia kutengeneza vitambulisho vya Taifa ambavyo vitakuwa na saini ya mwenye kitambulisho hicho na anayekitoa.
“Tumepokea maoni ya watu wengi wakionyesha umuhimu wa saini kwenye kitambulisho, kama Rais (John) Magufuli alivyosema. Kwa hiyo, tunakamilisha taratibu za kubadilisha kanuni ili vitambulisho tutakavyoendelea kuvitoa viwe na saini,” alisema.
Hata hivyo alisistiza kwamba vitambulisho ambavyo havina saini vitaendelea kutumika na kutambuliwa kwa sababu saini ipo kwenye nyaraka nyingine.
Alisema Nida itaruhusu pia wananchi kwenda kubadilisha na kupata vitambulisho vyenye saini.
Lengo la mabadilikp haya ni kuongeza ufanisi kwa uwajibikaji. Hasara iliyopatikana ni kubwa sana, hatutaki tuendelee kubeba msalaba huu wakati lengo kuu halijatimia,” alisema Dk Kipilimba.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.