Skip to main content

Mrithi wa Dk Slaa kujulikana leo


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - Chadema
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema
Katibu mkuu mpya wa Chadema atajulikana leo wakati Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe atakapowasilisha jina la mtu anayempendekeza kushika wadhifa huo.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalim alisema jana kuwa jina hilo linatarajiwa kuwasilishwa mbele ya kikao cha Baraza Kuu kinachoanza hapa leo.
Moshi mweupe kuhusu jina la katibu mkuu mpya utaonekana Jumamosi mchana (leo). Mimi na Naibu Katibu Mkuu mwenzangu John Mnyika tuko tayari kumpokea bosi mpya,” alisema Mwalimu.
Katika kikoa chake na waandishi wa habari kilichohudhuriwa na Mnyika, Kaimu Katibu Mkuu huyo alisema hadi sasa, hakuna yeyote miongoni mwa viongozi na wanachama wa Chadema anayejua kwa hakika nani atarithi mikoba hiyo iliyoachwa na Dk Willibrod Slaa zaidi ya Mbowe.
Alipoulizwa jana, Mbowe hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa undani zaidi ya kuahidi kumteua katibu mkuu atakayemudu kubeba dhamana ya kuivusha Chadema salama katika harakati za kushika dola katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Profesa Mwesiga Baregu alisema: “Tunaweza kufikia uamuzi kwa maridhiano bila hata wajumbe kulazimika kupiga kura. Hilo naweza kukuhakikishia kwa sababu mimi ndiye mwenyekiti wa kamati ya maridhiano.”
Pamoja na kupitisha jina la katibu mkuu, vikao vikuu vya Chadema ambavyo kwa mara ya kwanza vimefanyika nje ya Dar es Salaam, pia vinatarajiwa kujadili na kuamua mpango mkakati wa kisiasa wa miaka mitano kuanzia sasa hadi 2021, kupitisha bajeti ya chama kwa kipindi hicho na kufanya marekebisho ya
katiba, kanuni na miongozo ya mabaraza.
Umeya Dar
Wakati jana Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene akitangaza kwamba uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam utafanyika kabla ya Machi 25, Mwalimu na Mnyika walimsihi Rais John Magufuli kuingilia kati kuepusha balaa inayochochewa na wasaidizi wake akiwamo waziri huyo.
“Suala la uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ni jipu lililoko ndani ya Ikulu linalopaswa kutumbuliwa na Rais Magufuli mwenyewe kupitia nafasi yake ya Waziri wa Tamisemi kwa sababu wizara hii iko chini yake,” alisema Mnyika.
Wakati Chadema ikitoa malalamiko hayo, Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Juma Simba “Gadafi” amemuomba Waziri Simbachawene kuangalia utendaji wa kazi wa wakurugenzi wa Manispaa za Ilala na Kinondoni, akidai wamevuruga uchaguzi wa meya na naibu wake.
Akizungumza na wanahabari jana, Simba alisema CCM imefikia hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na utendaji kazi wa wakurugenzi hao, ikiwamo kushindwa kutafsiri vyema vifungu vya sheria vilivyosababisha kuondolewa kwa ya majina ya wajumbe wao kwa madai kuwa hawana sifa za kushiriki uchaguzi huo.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.