Skip to main content

Mrithi wa Dk Slaa bado siri ya Mbowe


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
Siri ya mtu atakayerithi nafasi ya katibu mkuu wa Chadema iliyoachwa wazi na Dk Willibrod Slaa, bado ni ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.
Kwa mujibu wa ibara ya 7 (13)(b) ya Katiba ya Chadema, mwenyekiti wa chama ndiye anayetakiwa kupendekeza majina mawili kwenye kikao cha Baraza Kuu ambacho hupiga kura kumchagua katibu mkuu kati ya wawili yao.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisa wa habari wa Chadema, Tumaini Makene juzi, kikao cha Baraza Kuu kitafanyika Machi 12 jijini Mwanza, kikitarajia kupokea majina hayo mawili na kuchagua mojawapo kwa ajili ya kuziba nafasi ya Dk Slaa aliyejiuzulu siasa za vyama tangu Septemba Mosi, 2015.
Kikao cha baraza hilo kitafuatiwa na Kamati Kuu Machi 13 na Machi 14 kutakuwa na kikao cha Sekretarieti.
“Bado natafakari suala hilo,” alisema Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa tatu wa Chadema tangu ianzishwe mwaka 1992.
Dk Slaa, ambaye aliibukia kuwa katibu mkuu mwenye ushawishi wa chama hicho kikuu cha upinzani, alijiondoa Chadema kwa madai kuwa ilikubali kumpokea Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kumpa fursa ya kugombea urais kabla ya kujisafisha dhidi ya tuhuma za ufisadi zilizokuwa zikimkabili.
Tangu Dk Slaa ajiondoe, nafasi yake imekuwa ikikaimiwa na Salum Mwalimu ambaye ni naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa Zanzibar.
Wakati Mbowe akitafakari majina hayo, tayari ubashiri unamtaja Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye kuwa mmoja wa watu wanaopewa nafasi kubwa ya kupendekezwa, sambamba na mnadhimu na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - Chadema
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema
Hata hivyo, Sumaye amekuwa akieleza kuwa hafikirii kushika nafasi hiyo kwa kuwa umri umeshakwenda na kwamba uamuzi wake wa kujiunga na chama hicho haukuwa wa kutafuta madaraka.
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Lissu hakutaka kuzungumzia uwezekano wa jina lake kupendekezwa, badala yake alijikita katika utaratibu wa kikatiba wa kujaza nafasi hiyo.
“Katibu mkuu anatakiwa awe mtu atakayesimamia heshima ndani ya chama, lazima awe mtu ambaye akisema kitu chama kinasikiliza na nchi inasikiliza. Pia awe mtu anayekifahamu chama,” alisema Lissu, ambaye pia ni mwanasheria wa kujitegemea.
“Awe na uwezo wa kuvaa viatu vya Dk Slaa ambavyo si vidogo, ni vikubwa kweli kweli.”
Dk Slaa alijizolea umaarufu kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi pamoja na kulipua mabomu kwenye Serikali ya Awamu ya Nne.
Mbunge huyo wa zamani wa Hanang’ alipitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili, nyuma ya Jakaya Kikwete.
Alikuwa akitajwa tena kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, lakini upepo ulibadilika baada ya Lowassa kujiondoa CCM akipinga mchakato wa kumpata mgombea urais wa chama hicho na kujiunga na Chadema.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...