Skip to main content

Mrithi wa Dk Slaa bado siri ya Mbowe


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
Siri ya mtu atakayerithi nafasi ya katibu mkuu wa Chadema iliyoachwa wazi na Dk Willibrod Slaa, bado ni ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.
Kwa mujibu wa ibara ya 7 (13)(b) ya Katiba ya Chadema, mwenyekiti wa chama ndiye anayetakiwa kupendekeza majina mawili kwenye kikao cha Baraza Kuu ambacho hupiga kura kumchagua katibu mkuu kati ya wawili yao.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisa wa habari wa Chadema, Tumaini Makene juzi, kikao cha Baraza Kuu kitafanyika Machi 12 jijini Mwanza, kikitarajia kupokea majina hayo mawili na kuchagua mojawapo kwa ajili ya kuziba nafasi ya Dk Slaa aliyejiuzulu siasa za vyama tangu Septemba Mosi, 2015.
Kikao cha baraza hilo kitafuatiwa na Kamati Kuu Machi 13 na Machi 14 kutakuwa na kikao cha Sekretarieti.
“Bado natafakari suala hilo,” alisema Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa tatu wa Chadema tangu ianzishwe mwaka 1992.
Dk Slaa, ambaye aliibukia kuwa katibu mkuu mwenye ushawishi wa chama hicho kikuu cha upinzani, alijiondoa Chadema kwa madai kuwa ilikubali kumpokea Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kumpa fursa ya kugombea urais kabla ya kujisafisha dhidi ya tuhuma za ufisadi zilizokuwa zikimkabili.
Tangu Dk Slaa ajiondoe, nafasi yake imekuwa ikikaimiwa na Salum Mwalimu ambaye ni naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa Zanzibar.
Wakati Mbowe akitafakari majina hayo, tayari ubashiri unamtaja Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye kuwa mmoja wa watu wanaopewa nafasi kubwa ya kupendekezwa, sambamba na mnadhimu na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - Chadema
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema
Hata hivyo, Sumaye amekuwa akieleza kuwa hafikirii kushika nafasi hiyo kwa kuwa umri umeshakwenda na kwamba uamuzi wake wa kujiunga na chama hicho haukuwa wa kutafuta madaraka.
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Lissu hakutaka kuzungumzia uwezekano wa jina lake kupendekezwa, badala yake alijikita katika utaratibu wa kikatiba wa kujaza nafasi hiyo.
“Katibu mkuu anatakiwa awe mtu atakayesimamia heshima ndani ya chama, lazima awe mtu ambaye akisema kitu chama kinasikiliza na nchi inasikiliza. Pia awe mtu anayekifahamu chama,” alisema Lissu, ambaye pia ni mwanasheria wa kujitegemea.
“Awe na uwezo wa kuvaa viatu vya Dk Slaa ambavyo si vidogo, ni vikubwa kweli kweli.”
Dk Slaa alijizolea umaarufu kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi pamoja na kulipua mabomu kwenye Serikali ya Awamu ya Nne.
Mbunge huyo wa zamani wa Hanang’ alipitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili, nyuma ya Jakaya Kikwete.
Alikuwa akitajwa tena kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, lakini upepo ulibadilika baada ya Lowassa kujiondoa CCM akipinga mchakato wa kumpata mgombea urais wa chama hicho na kujiunga na Chadema.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...