Skip to main content

Mrithi wa Dk Slaa bado siri ya Mbowe


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
Siri ya mtu atakayerithi nafasi ya katibu mkuu wa Chadema iliyoachwa wazi na Dk Willibrod Slaa, bado ni ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.
Kwa mujibu wa ibara ya 7 (13)(b) ya Katiba ya Chadema, mwenyekiti wa chama ndiye anayetakiwa kupendekeza majina mawili kwenye kikao cha Baraza Kuu ambacho hupiga kura kumchagua katibu mkuu kati ya wawili yao.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisa wa habari wa Chadema, Tumaini Makene juzi, kikao cha Baraza Kuu kitafanyika Machi 12 jijini Mwanza, kikitarajia kupokea majina hayo mawili na kuchagua mojawapo kwa ajili ya kuziba nafasi ya Dk Slaa aliyejiuzulu siasa za vyama tangu Septemba Mosi, 2015.
Kikao cha baraza hilo kitafuatiwa na Kamati Kuu Machi 13 na Machi 14 kutakuwa na kikao cha Sekretarieti.
“Bado natafakari suala hilo,” alisema Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa tatu wa Chadema tangu ianzishwe mwaka 1992.
Dk Slaa, ambaye aliibukia kuwa katibu mkuu mwenye ushawishi wa chama hicho kikuu cha upinzani, alijiondoa Chadema kwa madai kuwa ilikubali kumpokea Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kumpa fursa ya kugombea urais kabla ya kujisafisha dhidi ya tuhuma za ufisadi zilizokuwa zikimkabili.
Tangu Dk Slaa ajiondoe, nafasi yake imekuwa ikikaimiwa na Salum Mwalimu ambaye ni naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa Zanzibar.
Wakati Mbowe akitafakari majina hayo, tayari ubashiri unamtaja Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye kuwa mmoja wa watu wanaopewa nafasi kubwa ya kupendekezwa, sambamba na mnadhimu na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - Chadema
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema
Hata hivyo, Sumaye amekuwa akieleza kuwa hafikirii kushika nafasi hiyo kwa kuwa umri umeshakwenda na kwamba uamuzi wake wa kujiunga na chama hicho haukuwa wa kutafuta madaraka.
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Lissu hakutaka kuzungumzia uwezekano wa jina lake kupendekezwa, badala yake alijikita katika utaratibu wa kikatiba wa kujaza nafasi hiyo.
“Katibu mkuu anatakiwa awe mtu atakayesimamia heshima ndani ya chama, lazima awe mtu ambaye akisema kitu chama kinasikiliza na nchi inasikiliza. Pia awe mtu anayekifahamu chama,” alisema Lissu, ambaye pia ni mwanasheria wa kujitegemea.
“Awe na uwezo wa kuvaa viatu vya Dk Slaa ambavyo si vidogo, ni vikubwa kweli kweli.”
Dk Slaa alijizolea umaarufu kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi pamoja na kulipua mabomu kwenye Serikali ya Awamu ya Nne.
Mbunge huyo wa zamani wa Hanang’ alipitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Chadema mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili, nyuma ya Jakaya Kikwete.
Alikuwa akitajwa tena kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, lakini upepo ulibadilika baada ya Lowassa kujiondoa CCM akipinga mchakato wa kumpata mgombea urais wa chama hicho na kujiunga na Chadema.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.