Skip to main content

Je, haki itatendeka katika kesi inayomkabili Kenyatta ya uhalifu dhidi ya ubinadamu..?


Na Julius Kithuure, Nairobi
Huku kesi dhidi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai imeahirishwa kwa muda usiojulikana, watu wa Kenya wanatoa maoni mbalimbali kuhusu mwelekeo na namna nzuri ya kuona haki ikitendeka.
Mwandanamaji wa Kenya akiangalia picha za vurugu za baada ya uchaguzi wakati wa maandamano huko Nairobi mwaka 2011. [Simon Maina/AFP]
Ingawa kuna maoni tofauti, karibia kila mmoja ana kitu cha kusema kuhusu hili. Baadhi wanaunga mkono uahirishaji huo wa kesi hiyo, wakati wengine wanasema waendeshaji kesi wa ICC wanapaswa kustahimili. Wengine bado wanatoa wito kwa njia mbadala wa Kenya badala ya mahakama ya kimataifa.
Kesi dhidi ya Kenyatta katika ICC imekuwa na vizuizi mbalimbali kutoka ilipoanza, huku mashahidi mbalimbali wakiondoa ushahidi wao na madai kuwa ushahidi umechafuliwa na pande zote za kesi. Katika mwezi wa Disemba, Mwendesha Mashtaka wa ICC Fatou Bensouda alikiri kwamba hakuwa na ushahidi wa kutosha kumshtaki Kenyatta kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu wakati wa vurugu za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007 hadi 2008, na mnamo tarehe 23 Januari timu ya waendesha mashtaka iliomba kuahirisha kesi hiyo kwa muda usiojulikana.
Kenyatta ana masuala 'muhimu zaidi' ya kuzingatia
Wanaomuunga mkono Kenyatta wasema uendeshaji mashtaka unakosa ushahidi mzito na kuondolewa kwa ushahidi muhimu kumedhoofisha kabisa kesi hiyo.

Picha iliyochukuliwa tarehe 8 Aprili, 2011, ikionyesha Naibu Waziri Mkuu wa Kenya na Waziri wa Fedha Uhuru Kenyatta wa wakati huo (wa pili kushoto) kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai. [AFP]
"Ni wazi kwamba sasa kesi dhidi ya raisi huyu ni yenye kasoro na yenye kiasi kidogo cha uuaji," mbunge wa Juja Francis Munyua Waititu aliiambia Sabahi. "Basi ni kwa nini rais apoteze nguvu zake, muda na rasilimali kwa suala ambalo halina kichwa wala mkia?"

Comments