Skip to main content

ORYX YA GAWA VITABU SHELE YA MSINGI BOMA

io WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Boma Wilaya ya Ilala wakiigiza igizo lao kwa mgeni rasimi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaaam Jana mchana , ambapo igizo hilo lilionekana kuwa na mvuto likizungumzia baadhi ya mandhari ya shule yao kuhusu wamachinga waano pita njia ya Shuleni kwao wakati wa masomo kutokana na kuta ya kuzia kuwa imeanguka na hivyo kuwa na kero kwao katika masomo.




MTANGAZAJI wa Radio Clouds FM , FM Kibonde akiwa ndiye mc katika hafla fupi iliyo andaliwa na Kampuni ya Oryx kwa ajili ya kugawa vitabu vya mitaala kwa baadhi ya wanafunzi wa Shule za Msingi za Dar es Salaaam jana katika hafla fupi iliyofanyika mchana kwenye shule ya msingi Boma iliyoko katika Wilaya ya Ilala.
KUU wa Mkoa akiwa katika hutuba yake kwa baadhi ya Walimu wa Dar es Salaam janakwenye Shule ya Msingi Boma Ilala .
MKUU wa mkoa wa Dar es Salaam Wiliam Lukuvi akipokelewa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Boma , jana mchana , alipokwenda kukabidhi vitabu vya mitaala ya masomo vilivyotolewa na kamupuni ni ya Oryx.





WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Boma wakimlaki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Wiliam Lukuvi jana.

HAPA ulikuwa muda wa saa nne asubuhi kabla ya Mkuu wa Mkoa kufika Shuleni hapo ambapo wanafunzi hao walisema kuwa huwa wanakunywa Uji wenye kuwekewa sukari kwa kuuziwa kila kikombe shilingi 100 hali inayowafanya kurudi Darasani kuzingatia masomo kwa umakini mkubwa..

Comments