Skip to main content

Soma matarajio ya Yanga



KLABU ya Yanga inatarajia kuandaa hafla ya kuchangisha michango kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wake mpya wa kisasa maeneo ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam.

Habari kutoka ndani ya klabu hiyo zimeeleza kuwa, mgeni rasmi katika hafla hiyo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Jakaya Kikwete.

Kwa mujibu wa habari hizo, uamuzi wa kuandaa hafla hiyo ulifikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo kilichofanyika hivi karibuni mjini Dar es Salaam.

"Kamati ya utendaji iliyokutana hivi karibuni ilikubaliana kuandaa hafla kubwa ya kuchangisha mamilioni ya pesa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo,"alisema mmoja wa viongozi wa kamati hiyo, ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.

Mbali ya kuandaa hafla hiyo, kamati hiyo imeshapendekeza ramani ya uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 40,000, ambao ujenzi wake unatarajiwa kugharimu dola milioni 50 za Marekani

Chanzo hicho cha habari kilieleza kuwa, uwanja huo ndio chaguo la kwanza katika ramani zilizochorwa na kuwasilishwa kwa uongozi wa Yanga na Kampuni ya Beijing Construction Engineering tawi la Tanzania.

Kiliongeza kuwa, chaguo la pili ni uwanja ambao ujenzi wake utagharimu dola milioni 40 na wa tatu ujenzi wake utagharimu dola milioni 30.

Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema, anachojua ni kwamba mchakato wa ujenzi wa uwanja huo bado unaendelea.

"Mambo yatakakapokamilika, uongozi utaweka wazi kila kitu kwani muda si mrefu, ndoto ya klabu yetu kumiliki uwanja wa kisasa itakamilika,"alisema.

Mwezi uliopita, Kampuni ya Beijing Construction Engineering tawi la Tanzania, kupitia Meneja Msaidizi wake, Zhang Chengwei alisema, ujenzi wa uwanja huo utaanza mara baada ya uongozi wa Yanga kupata fedha.

Chengwei alisema uwanja huo utakuwa na sehemu ya maduka, hoteli, migahawa, 'super market', sehemu ya maegesho ya magari na uwanja mdogo wa mazoezi.

Alisema iwapo Yanga itakuwa na fedha za kutosha, watajenga uwanja huo kwa kipindi cha mwaka mmoja na utafanana na uwanja uliojengwa na kampuni hiyo nchini Afrika Kusini.

Kampuni hiyo ndiyo iliyojenga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Uwanja wa Uhuru, jengo la maonyesho la Chuo Kikuu cha Elimu (DUCE), uwanja wa ndege wa Zanzibar, jengo la mapumziko la wageni mashuhuri katika uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere na ofisi za Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA).Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...