Skip to main content

Kitengo cha kukabili ugaidi kuwasili mitaa ya Mogadishu


Na Adnan Hussein, Mogadishu
Serikali ya shirikisho ya Somalia imeunda na kukipa mafunzo kikosi maalumu cha askari kufanya operesheni dhidi ya ugaidi huko Mogadishu na kuzuia mipango ya al-Shabaab ya kulipua mabomu ya kujitoa muhanga kwa siku zijazo.
Askari wa Jeshi la Taifa la Somalia wakitembea wakati wa gwaride la jeshi tarehe 14 Aprili huko Mogadishu. Serikali ya shirikisho inaandaa kikosi maalum imara 1,000 waliopewa mafunzo kwa ajili ya operesheni dhidi ya ugaidi kusambazwa katika mji mkuu huo. [Na Stuart Price/AU-UN IST PHOTO/AFP]
Serikali inapanga kusambaza kikosi imara 1,000 ifikapo mwishoni mwa Aprili, kitakachojumuisha vikosi kutoka matawi kadhaa ya vikosi vya jeshi na vikosi vya usalama kwa mujibu wa Mohamud Ahmed Hirsi, meneja katika idara ya ugavi na usafirishaji wa watu na vitu wa Jeshi la Ulinzi la Somalia.
Kikosi hiki kitabomoa na kuharibu ngome za ugaidi na maficho, kuondoa kabisa operesheni zao na kutegua mabomu, katika jitihada za kurejesha amani na kanuni katika mji mkuu.
"Vikosi hivi vinawajibika kutafuta magaidi na wale wanaotuhumiwa kujihusisha katika operesheni za uuaji kwa sababu za kisiasa dhidi ya wahamasishaji amani, waandishi wa habari, polisi na maofisa wa jeshi," Hirsi aliiambia Sabahi. "Miongoni mwa malengo yake ni kushambulia vikundi vya kigaidi ambavyo vinafanya mauaji, wizi na kuiba mapato, pamoja na kuingilia mali binafsi, taasisi za serikali na migahawa."
Askari wa Jeshi la Taifa la Somalia wakishiriki katika mazoezi ya mafunzo tarehe 28 Machi katika kambi ya mafunzo ya Jazeera huko Mogadishu, mahali ambapo wakufunzi wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia wanaendesha vikosi vya Somalia kwa njia ya upangaji mpana wa ufundishaji askari na mbinu za kijeshi. [Na Tobin Jones/AU-UN IST PHOTO/AFP]
Baadhi ya vikosi kutoka katika kikosi kipya vitafanya doria kwenye maeneo ya mji ambako waasi wamejulikana kujificha, vikitekeleza hatua kali za ulinzi, Hirsi alisema. 
Vikosi vingine vitalinda usalama wa vituo vya ukaguzi vya kando ya barabara mahali pengine popote katika mji mkuu wakiwataka waendesha magari na pikipiki kuonyesha vitambulisho na kukabidhi magari yao kwa ukaguzi wa usalama.

Comments