Skip to main content

MSOME AFANDE SELE





MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Selemani Msindi 'Afande Sele' amegeuka muhubiri wa amani nchini baada ya kuibuka na kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la Dini tumeletewa.

Katika kibao chake hicho, Sele anazungumzia umuhimu wa Watanzania kuheshimiana licha ya kila mtu kuwa na dini yake, kabila lake na imani yake.

Akizungumza kwa njia ya simu wiki hii kutoka Morogoro, Sele alisema watanzania wanapaswa kuishi kwa amani na upendo kwa sababu dini ni kitu kilicholetwa na wageni kutoka nje.

Alisema tangu enzi na enzi, upendo, umoja na ushirikiano ndiyo dini ya watanzania hivyo wanapaswa kuiendeleza.

"Kabla ya ukoloni, wazee wetu waliishi kwa upendo, hawakuwa na dini, walisali popote na Mungu aliitikia sala zao. Walimwamini Mungu ndio kama ulimwengu, hakukuwa na kanisa wala msikiti, "alisema Sele.

"Walisali sala zao kwa miungu yao, dua zao silisikika kabla ya mwaka kumalizika, mvua kubwa ilinyesha hata kama sio masika,"aliongeza msanii huyo, ambaye aliwahi kutwaa taji la mfalme wa mashairi.

"Miaka inavyokwenda, dini zinaongezeka, nyingine toka mashariki ya mbali. Yule anajiona sahihi kuliko mwingine. Wenyewe kwa wenyewe tunaitana makafiri, dini zinasababisha ndugu kwa ndugu tunauana, ndugu wa baba na mama tunauana, kisa yule anaitwa Salehe mwingine Willy, Waafrika tunaonekana hatuna amani,"alisema msanii huyo.

Afande Sele alisema siku zote Mungu ni yule yule, isipokuwa majina ya wanaomwabudu ndiyo yanayotofautiana, ambapo kuna wengine wanaomwita Jah, Allah, Maulana, subhana na Jehova.

Alisema iwapo wazungu wasingekuja barani Afrika kutangaza dini zao, waafrika wote wangeitwa wapagani kwa sababu wasingekuwa na dini zaidi ya kuabudu dini zao za asili.

Msanii huyo alijifananisha na Nabii Suleiman na kudai kuwa, ameletwa nchini kwa ajili ya kuhubiri amani hivyo aliwataka watanzania kuwa makini katika kipindi hiki, ambacho zimeanza kujitokeza chokochoko za kidini.

Afande Sele alisema kibao cha Dini tumeletewa ni miongoni mwa vibao sita vitakavyokuwemo kwenye albamu yake mpya, anayotarajia kuitoa hivi karibuni. Alisema albamu hiyo itajulikana kwa jina la wimbo huo.

Afande Sele alisema licha ya mauzo ya albamu kwa wasanii nchini kwa sasa kusuasua, hatajali mauzo ya albamu yake hiyo mpya yatakuwaje.

"Lengo langu ni kuielimisha jamii, sio kupata maslahi. Sitofikiria soko kama litalipa au vipi, ninachohitaji ni kuwapa elimu watanzania,"alisema msanii huyo aliyetengeneza nywele zake kwa mtindo wa rasta.

Msanii huyo amewahi kurekodi vibao vingi, ambavyo vilimpatia sifa na umaarufu kutokana na ujumbe wake kugusa maisha ya kila siku ya jamii.

Baadhi ya vibao hivyo ni Mkuki moyoni, Kama nikipata ukimwi, Ndugu zangu, Mtu na pesa, Darubini kali, Malaria na nafasi ya mtu.

Mapema mwaka jana, Afande Sele alidokeza kuwa anatarajia kugombea mojawapo ya nafasi kubwa za kisiasa katika uchaguzi mkuu wa 2015. Japokuwa hakutaka kuitaja nafasi hiyo, lakini kuna habari kuwa amepanga kuwania ubunge.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...