Skip to main content

KOCHA YANGA : MECHI ZOTE ZILIZOSALIA KWETU NI FAINALI



KOCHA Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ametamba kuwa, mechi zote zilizosalia katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara kwao ni sawa na fainali hivyo hawawezi kuzipuuza.

Brandts alisema hayo baada ya mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika juzi kwenye uwanja wa Mabatini uliopo Kijitonyama, Dar es Salaam.

Kocha huyo alisema wanaipa uzito mkubwa mechi kati yao na Ruvu Shooting itakayochezwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa vile wapinzani wao si timu ya kubeza.

Katika mechi ya kwanza kati ya timu hizo iliyochezwa Oktoba 20 mwaka jana, Yanga iliichapa Ruvu Shooting mabao 3-2.

Yanga inaongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 45 baada ya kucheza mechi 19 wakati Ruvu Shooting inashika nafasi ya sita ikiwa na pointi 29 baada ya kucheza mechi 18.

"Ninakiandaa kikosi changu kuhakikisha kinapata pointi tatu katika kila mchezo ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa,"alisema Brandts.

"Kila mchezo tunaocheza kwa sasa ni fainali kwetu, kila timu inahitaji kupata pointi ili kujiweka katika nafasi nzuri, na sisi pia tunahitaji kupata pointi tatu katika kila mchezo. Nadhani mechi itakuwa ngumu,"aliongeza kocha huyo.

Katika mechi yake iliyopita, Yanga iliwalaza ndugu zao wa Toto African bao 1-0. Mechi hiyo ilipigwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wakati huo huo, daktari wa Yanga, Nassoro Matuzya amesema wachezaji Kevin Yondan na Saidi Bahanuzi wameanza mazoezi na wenzao baada ya kuwa majeruhi kwa siku kadhaa.

Nassoro alisema Yondan alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya kidole gumba, aliyoyapata katika mechi dhidi ya Toto African wakati Bahanuzi alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya msuli wa kisigino.

Daktari huyo alisema pia kuwa, beki Ladislaus Mbogo ameshafanyiwa upasuaji wa uvimbe shavuni na hali yake inaendelea vizuri.Chanzo kimoja kimeeleza.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...