Skip to main content

Ebu Msome NYoni!


KIUNGO Erasto Nyoni wa timu ya ‘wauza koni’ wa Azam FC, amesema kanuni iliyorejeshwa msimu huu na Shirikisho la Soka, TFF, ya kuzitaka klabu za ligi kuu ya Bara kutosajili wachezaji wa kigeni zaidi ya watano ni nzuri kwani itasaidia ligi hiyo kuwa na wageni ngangari.

Nyoni aliyewahi pia kuwa mchezaji wa kigeni katika ligi kuu ya Burundi wakati akikipiga katika klabu ya Vital ‘O ya Bujumbura msimu wa 2006, aliiambia Lete RAHA jana Jumamosi kuwa, kurejeshwa kwa kanuni hiyo kutazilazimisha timu zote kusajili ‘vifaa’ vya ukweli, na si kupapatikia majina makubwa ya wageni ‘waliofulia’ na wasio na kiwango bora uwanjani.

"Mimi naamini uamuzi wa kutumiwa kwa kanuni hii una faida nyingi kuliko hasara zinazolalamikiwa na baadhi ya watu… kwa sababu wageni wanaoruhusiwa ni watano pekee, naamini kila timu itahakikisha kuwa inawasajili wachezaji wakali na ambao hawataishia kuwa watazamaji majukwaani huku mwisho wa siku wakilipwa fedha nyingi.

"Kwa sababu hiyo, ushindani wa kuwania kupangwa katika kila timu na pia ule wa ndani ya uwanja wakati wa mechi utaongezeka. Mwishowe kiwango chetu kitapanda," anasema Nyoni, ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wachezaji waliokuwa wakiibeba timu ya taifa, Taifa Stars, wakati ilipokuwa chini ya kocha aliyemaliza mkataba wake mwezi uliopita, Mbrazili Marcio Maximo.

"Faida nyingine ni kwamba, wageni legelege hawatawazibia nafasi wachezaji chipukizi katika usajili. Hili litawasaidia wadogo wenye vipaji kupata nafasi ya kucheza na pengine kuitwa katika timu ya taifa ili baadaye wasaidie katika kuunda kikosi kikali cha nyota chipukizi kama ilivyokuwa kwa timu zilizojaza yosso wengi za Ghana na Ujerumani katika fainali za Kombe la Dunia.

"Enzi za kusajili wageni wenye majina maarufu, lakini wasiokuwa na kiwango kinachoendana na sifa na bei wanazonunuliwa sasa zitafikia mwisho. Azam husajili wageni wakali tupu na kuna programu nzuri za kukuza vijana ambao baadaye hupandishwa katika timu kubwa.

"Ni kwa sababu kama hizi, zinazosaidia kukua kwa kiwango cha soka nchini, ndipo binafsi ninapoona kwamba TFF iko sahihi kuishikia bango kanuni hiyo inayokataza timu za ligi kuu kusajili wageni zaidi ya watano," anasema Nyoni, mkali aliyevutiwa na kiungo ‘yosso’ Dede Ayew wa Ghana kutokana na kiwango cha juu alichoonyesha wakati wa fainali za Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini; lakini aliyekerwa na utabiri wa pweza Paul katika mechi ya fainali ambao ulikuwa wa kweli na hatimaye kuipa ubingwa Hispania dhidi ya timu aliyotarajia itwae kombe hilo ya Uholanzi.

AGOSTI 21

Nyoni anasema katika msimu ujao wa ligi kuu ya Bara itakayoanza kutimua vumbi Agosti 21, kwa mara ya kwanza, klabu yake ya Azam iliyomaliza katika nafasi ya tatu msimu uliopita baada ya kuzidiwa na timu za Simba na Yanga, itamaliza tambo za klabu hizo kongwe kwa kutwaa ubingwa wa 2010/2011.

Akifafanua sababu za kuwa na matumaini hayo, Nyoni anasema kuwa timu yao (Azam) imesajili kikosi cha mwaka huu kwa umakini zaidi kulinganisha na wapinzani wao wote na kwamba kama ni ‘fitna’, haamini kuwa zitawakwaza uwanjani kutokana na maandalizi yao makali katika fukwe za peninsula ya Kigamboni na pia visiwani Zanzibar.

"Kama nilivyosema awali, timu yetu inaangalia zaidi uwezo wa wachezaji na si majina yao. Kila aliyejumuishwa kikosini, ameangaliwa kwa uwezo wake na maandalizi yetu ndiyo yanayonipa imani zaidi kwamba ubingwa wa msimu ujao utaangukia mikononi mwetu," anasema Nyoni, pengine akikunwa na yosso tele wenye vipaji kikosini mwao na pia usajili wao mpya uliowaleta klabuni kwao nyota kadhaa, wakiwemo Mrisho Ngassa kutoka Yanga, Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na Jabiri Aziz kutoka Simba na Patrick Mafisango kutoka kwa mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, klabu ya APR ya Rwanda.

chanzi ni mtandao wa Azam football club na Habari kwa hisani ya Gazeti la LeteRaha

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...