Skip to main content

Ebu Msome NYoni!


KIUNGO Erasto Nyoni wa timu ya ‘wauza koni’ wa Azam FC, amesema kanuni iliyorejeshwa msimu huu na Shirikisho la Soka, TFF, ya kuzitaka klabu za ligi kuu ya Bara kutosajili wachezaji wa kigeni zaidi ya watano ni nzuri kwani itasaidia ligi hiyo kuwa na wageni ngangari.

Nyoni aliyewahi pia kuwa mchezaji wa kigeni katika ligi kuu ya Burundi wakati akikipiga katika klabu ya Vital ‘O ya Bujumbura msimu wa 2006, aliiambia Lete RAHA jana Jumamosi kuwa, kurejeshwa kwa kanuni hiyo kutazilazimisha timu zote kusajili ‘vifaa’ vya ukweli, na si kupapatikia majina makubwa ya wageni ‘waliofulia’ na wasio na kiwango bora uwanjani.

"Mimi naamini uamuzi wa kutumiwa kwa kanuni hii una faida nyingi kuliko hasara zinazolalamikiwa na baadhi ya watu… kwa sababu wageni wanaoruhusiwa ni watano pekee, naamini kila timu itahakikisha kuwa inawasajili wachezaji wakali na ambao hawataishia kuwa watazamaji majukwaani huku mwisho wa siku wakilipwa fedha nyingi.

"Kwa sababu hiyo, ushindani wa kuwania kupangwa katika kila timu na pia ule wa ndani ya uwanja wakati wa mechi utaongezeka. Mwishowe kiwango chetu kitapanda," anasema Nyoni, ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wachezaji waliokuwa wakiibeba timu ya taifa, Taifa Stars, wakati ilipokuwa chini ya kocha aliyemaliza mkataba wake mwezi uliopita, Mbrazili Marcio Maximo.

"Faida nyingine ni kwamba, wageni legelege hawatawazibia nafasi wachezaji chipukizi katika usajili. Hili litawasaidia wadogo wenye vipaji kupata nafasi ya kucheza na pengine kuitwa katika timu ya taifa ili baadaye wasaidie katika kuunda kikosi kikali cha nyota chipukizi kama ilivyokuwa kwa timu zilizojaza yosso wengi za Ghana na Ujerumani katika fainali za Kombe la Dunia.

"Enzi za kusajili wageni wenye majina maarufu, lakini wasiokuwa na kiwango kinachoendana na sifa na bei wanazonunuliwa sasa zitafikia mwisho. Azam husajili wageni wakali tupu na kuna programu nzuri za kukuza vijana ambao baadaye hupandishwa katika timu kubwa.

"Ni kwa sababu kama hizi, zinazosaidia kukua kwa kiwango cha soka nchini, ndipo binafsi ninapoona kwamba TFF iko sahihi kuishikia bango kanuni hiyo inayokataza timu za ligi kuu kusajili wageni zaidi ya watano," anasema Nyoni, mkali aliyevutiwa na kiungo ‘yosso’ Dede Ayew wa Ghana kutokana na kiwango cha juu alichoonyesha wakati wa fainali za Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini; lakini aliyekerwa na utabiri wa pweza Paul katika mechi ya fainali ambao ulikuwa wa kweli na hatimaye kuipa ubingwa Hispania dhidi ya timu aliyotarajia itwae kombe hilo ya Uholanzi.

AGOSTI 21

Nyoni anasema katika msimu ujao wa ligi kuu ya Bara itakayoanza kutimua vumbi Agosti 21, kwa mara ya kwanza, klabu yake ya Azam iliyomaliza katika nafasi ya tatu msimu uliopita baada ya kuzidiwa na timu za Simba na Yanga, itamaliza tambo za klabu hizo kongwe kwa kutwaa ubingwa wa 2010/2011.

Akifafanua sababu za kuwa na matumaini hayo, Nyoni anasema kuwa timu yao (Azam) imesajili kikosi cha mwaka huu kwa umakini zaidi kulinganisha na wapinzani wao wote na kwamba kama ni ‘fitna’, haamini kuwa zitawakwaza uwanjani kutokana na maandalizi yao makali katika fukwe za peninsula ya Kigamboni na pia visiwani Zanzibar.

"Kama nilivyosema awali, timu yetu inaangalia zaidi uwezo wa wachezaji na si majina yao. Kila aliyejumuishwa kikosini, ameangaliwa kwa uwezo wake na maandalizi yetu ndiyo yanayonipa imani zaidi kwamba ubingwa wa msimu ujao utaangukia mikononi mwetu," anasema Nyoni, pengine akikunwa na yosso tele wenye vipaji kikosini mwao na pia usajili wao mpya uliowaleta klabuni kwao nyota kadhaa, wakiwemo Mrisho Ngassa kutoka Yanga, Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na Jabiri Aziz kutoka Simba na Patrick Mafisango kutoka kwa mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, klabu ya APR ya Rwanda.

chanzi ni mtandao wa Azam football club na Habari kwa hisani ya Gazeti la LeteRaha

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...